Tetesi zinasema, Newcastle huenda wakatumia hadi pauni milioni 190 kumpata mshambuliaji wa Tottenham na England Harry Kane, 28, na mshambuliaji wa Ufaransa Kylian Mbappe, 22.
Tetesi zinasema, Kocha wa zamani wa Chelsea, Antonio Conte anaweza kuchukua nafasi ya Steve Bruce katika klabu ya Newcastle baada ya mwekezaji mpya kununua klabu hiyo.
Tetesi zinasema, Philippe Coutinho, 29, huenda akatua uwanja wa St James’ Park kutoka Barcelona mwezi Januari.

Kiungo wa kati wa Portugal Bruno Fernandes, 27, amekuwa akiwasiliana na mchezaji nyota wa nyota wa Leeds Mbrazil Raphinha, 24, kuhusu uwezekano wa kuhamia Manchester United.
Tetesi zinasema, Mshambuliaji wa zamani wa Newcastle Demba Ba, 36, amejitolea kurejea tena kuchezea klabu hiyo baada ya kununuliwa.
Beki wa Ujerumani Antonio Rudiger, 28, ni chaguo la kwanza la Real Madrid mwakani, kandarasi yake na Chelsea ikitarajiwa kukamilika msimu huu wa joto.
Kiungo wa kati wa England Ainsley Maitland-Niles, 24, na kiungo wa kati wa Misri Mohamed Elneny, 29, huenda wakaondoka Arsenal kwenda kusaka nafasi ya kucheza soka ya safu ya kwanza mwezi Januari.

Mshambuliaji wa Argentina Sergio Aguero, 33, alikataa ombi la Juventus kutaka ajiunge nao kabla ya kwenda Barcelona kwa uhamisho wa bure baada ya kuondoka Manchester City msimu wa kiangazi.
Juventus wanapanga kumuuza kiungo wa kati wa Wales Aaron Ramsey, 30, Januari mwakani, huku West Ham na Everton wakionesha nia ya kutaka kumnunua.
SPACE SPIN NA MERIDIANBET.
Ni Mabingwa pekee Meridianbet wanakupa nafasi ya kushinda zaidi na mchezo wa Space Spin katika kasino bomba za meridianbet. Ni wakati wa kufurahia na kutengeza mkwanja bila kuwaza.


