Kocha wa klabu ya Valencia Jose Bordalas ameihoji La Liga kuhusu sheria ya “Fair Play” inafanyaje kazi kutokana na sakata la usajiri wa Ferran Torres
Barcelona wamekamilisha usajiri wa Ferran Torres katika dirisha hili lilofunguliwa mwezi huu, ingawa bado hawajamsajiri kwenye hati ya malipo ya mishahara kutokana na sheria za La Liga za ukomo wa malipo wakati klabu ya Valencia haiwezi kusajiri kutokana kuwa kwenye tatizo sawa na Barcelona.

Kwa hali waliyona klabu ya Barcelona ilikuwa ngumu kwao kuweza kufanya usajiri wa pesa nyingi namna ile, na hicho ndicho Jose Bordalas alihoji kwenye mkutano wake na waandishi wa habari.
Barcelona wana deni la EURO 300 million na wamemsajiri Ferran Torres, haki ya mchezo uko wapi?
Jose Bordalas
Sababu ambayo Barcelona wameweza kufanya usajiri mkubwa wa kumsajiri Torres ni baada ya kuchukua mkopo mkubwa hivi karibuni
Ingawa klabu ya Barcelona wameweza kupunguza kiwango chwa mishara kwenye hati ya malipo msimu huu, kutokana na matumizi makubwa na kupungua kwa faida Barc hawawezi kumsajiri Torres mpaka waruhusu kuuza baadhi ya wachezaji.
Una Kila sababu ya kufurahia wiki yako na kutengeneza mwaka huu uwe wa faida zaidi katika kasino zetu za mtandaoni za meridianbettz. Mchezo wa Zeus Ancient Fortunes unakuongoza kutekeleza hilo.


