Kunako muendelezo wa NBA, timu ya Miami Heats imewaadhibu vinara wa Western Conference – Utah Jazz.
Jazz ambaye anatamba kwa ushindi wa michezo 22 kati ya 24, wamejikuta wakiangukia pua mikononi mwa Heats jana usiku.
Jimmy Butler alipachika pointi 33 huku swahiba wake Goran Dragic ambaye alipachika pointi 26 akitokea benchi katika mchezo ambao Jazz amepoteza kwa pointi 124-116. Huu ni ushindi wa 5 mfululizo kwa Miami Heats msimu huu ikiwa ni kipigo cha 3 kwa Jazz.
Kwingineko kunako NBA, LA Lakers wamepindua meza baada ya kupoteza michezo 4 mfululizo. Lakers waliwaadhibu Portland Trail Blazzers. LeBron James alipachika pointi 28, alitoa pasi 7 na kucheza mipira 11 iliyopotea.

Matokeo ya michezo ya NBA iliyochezwa Ijumaa usiku: Boston Celtics 118-112 Indiana Pacers, Toronto Raptors 122-111 Houston Rockets, Sacramento Kings 110-107 Detroit Pistons, Phoenix Suns 106-97 Chicago Bulls, Los Angeles Clippers 119-99 Memphis Grizzlies, Oklahoma City Thunder 118-109 Atlanta Hawks, Golden State Warriors 130-121 Charlotte Hornets na Los Angeles Lakers 102-93 Portland Trail Blazers
BusttheBank ni sloti inayokupa Mkwanja wa kutosha. Ndio, hii ni sloti inayokupa faida ya hadi mara kibao ya dau lako. Ni Meridianbettz pekee utakapoweza kupata burudani hii.
Pole sana Jazz
Poleyenu jazz
Pole Sana
Asante kwa taarifa
Pole sana
Pole sana
Duh pole yao
Pole
Kaz kazin
Miami zao ni kipigo tu