Usiku wa kuamkia Jumapili Tyson Fury atakabiliana na bondia Deontay Wilder likiwa ni pambano lao la tatu baada ya kupigana hapo nyuma na Fury kushinda mapambano yote mawili, sasa kuelekea pambano lao wamepima uzito na Fury ameonekana amemzidi mpinzani wake kilogram 20.

Fury atakuwa akitetea mkanda wake wa WBC dhidi ya Wilder ambaye atakuwa na fursa nyingine ya kujiuliza alikuwa akikosea wapi.
Wilder alipima na kupatikana na kg 107 wakati bondia kutoka Uingereza Fury alikuwa na kg 127.
Ikumbukwe katika pambano lao la kwanza Wilder alikuwa na kiligramu 96 wakati huo Fury alikuwa kilogramu 116, vilevile katika pambano lao la pili Wilder alikuwa amefikisha kg 104 wakati Fury alikuwa na uzito wa kg 123.
SPACE SPIN NA MERIDIANBET.
Ni Mabingwa pekee Meridianbet wanakupa nafasi ya kushinda zaidi na mchezo wa Space Spin katika kasino bomba za meridianbet. Ni wakati wa kufurahia na kutengeza mkwanja bila kuwaza.


