Ansu Fati alikuwa akitarajia kucheza mchezo wake wa kwanza dhidi ya Granada siku ya Jumatatu baada ya kukaa nje ya dimba kwa miezi 10 sababu ya jeraha alilopata lakini imekuwa ni mapema sana kwa kinda huyo na kupelekea kuondolewa kwenye kikosi cha Barcelona.

Lakini The Blaugrana wanatumaini la kupata huduma ya kinda huyo wa miaka 18 kwenye mchezo wa LaLiga dhidi ya Cadiz siku ya Alhamisi ijayo.
Wote kocha na timu ya matibabu wanataka kwenda hatua kwa hatua mpaka Ansu Fati awe sawa sawa kufuatia kufanyiwa operesheni tatu kwenye mguu wake.
Goti la Fati sasa linaendelea vizuri na malengo sasa ni kumpatia kujiamini na kurejea kwenye njia yake ya utupiaji mabao tena.
Mwanzoni iliionekena Ansu Fati anaweza kucheza mchezo wake katika wiki ya nne ya LaLiga kwa mechi ya Barca dhidi ya Sevilla mchezo ambao ulihairishwa wiki iliyopita.
Unaanzaje siku yako na kuimaliza bila kupitia katika kasino bomba za meridianbettz, mchezo mashuhuri wa Disco Funk unaweza kukufanya uwe mshindi leo hii.!