Timu ya taifa ya Ubeligiji imekata tiketi ya kwenda nchini Qatar kwaajili ya michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2022 baada ya kuinyuka Estonia 3-1 siku ya Jumamosi.
Katika mchezo huo Eden Hazard alianza lakini nafasi yake ilichukuliwa na mdogo wake Thorgan Hazard ambaye baadaye alifunga katika ushindi huo mnono lakini pia Yannick Carrasco aliweka kambani vilevile Christian Benteke alifunga bao la ufunguzi.
?Erik Sorga aliifungia Estonia bao la kufuatia machozi, ushindi huo ulimaanisha Belgium wamepata alama 19 kutoka michezo saba alama 5 mbele ya Wales ambao wanapointi 14 licha ya kushinda dhidi ya Belarus.
Unawezaje kuikosa hii! njia rahisi ya kutengeneza mkwanja katika kasino maridhawa za meridianbet. Muda wa kufurahia na kutengeneza mkwanja ipo mikononi mwako unasubiri nini?


