Kocha mkuu wa Barcelona Xavi Hernandez anataka kukijenga upya kikosi chake baada ya kuchaguliwa rasmi kuwa kocha wa mkuu mapema hii kufuatia kutimuliwa kwa aliyekuwa kocha mkuu wa The Blaugrana Ronald Koeman.

Dirisha la usajili la mwezi Januari litakuwa bize kwa Xavi na Barcelona wakiripotiwa kuhitaji huduma za wachezaji wa Chelsea ambapo wanataka dili ya mkopo kwa wachezaji Hakim Ziyech, Christian Pulisic na Callum Hudson-Odoi.
Kwa mujibu wa Diario Sport, Barcelona inatizamia kuwa sajili wachezaji hao watatu ambao wamekuwa wakipambana kupata muda wa kucheza chini ya mwalimu Thomas Tuchel na wanaonekana watakuwa wazuri katika eneo la ushambuliaji kwenye kikosi cha Xavi.
Xavi tayari amemleta mchezaji mwenzake wa zamani Dani Alves katika kikosi chake pia amehusishwa kumleta Camp Nou mchezaji wa zamani wa Barca na sasa Liverpool Thago Alcantara.
Tutaona mabadiliko makubwa kwenye nusu ya pili ya msimu katika kikosi cha Barcelona ambapo Xavi amepewa kazi ya kusimamia tiimu hiyo.
Unawezaje kuikosa hii! njia rahisi ya kutengeneza mkwanja katika kasino maridhawa za meridianbet. Muda wa kufurahia na kutengeneza mkwanja ipo mikononi mwako unasubiri nini?


