Imefichuka mabosi wa Chelsea wameingia upya kwenye sakata la kuiwania saini ya kiungo wa West Ham United na timu ya taifa ya England, Declan Rice katika dirisha lijalo la majira ya Kiangazi.
Katika mchakato huo mpya, Chelsea inafikiria kumtumia Tammy Abraham, 26, kama sehemu ya mabadilishano kisha iweke na kiasi cha pesa.
Rice, 22, ni miongoni mwa wachezaji wanaowindwa sana dirisha lijalo kwani mbali ya Chelsea, Manchester United na Manchester City zimekuwa zikijiandaa vyema kuhakikisha zinampata fundi huyo.
Mkataba wa sasa wa Rice unatarajiwa kumaliza mwaka 2024. West Ham ipo tayari kumuuza lakini kwa kiasi kisichopungua Pauni 90 milioni (Sh 296 Bilioni).
Bonasi ya 50% Kila Siku Katika Kasino za Evoplay hapa Meridianbet.
Meridianbet na Evoplay Kasino wanakupa bonasi ya 50% ya kiasi utakachoweka katika akaunti yako leo. Unasubiri nini ni wakati wa kupiga pesa sasa na Mabingwa.
Nice update