Droo ya hatua ya mtoano ya Kombe la Dunia la 2022 imepelekea Ureno na Italia kuwekwa kwenye kundi C la mtoano, kumaanisha kuwa mmoja kati ya wawili hao hatafuzu fainali za Kpmbe la Dunia nchini Qatar 2022.

Ureno itamenyana na Uturuki huku Italia ikimenyana na Macedonia Kaskazini katika mechi za nusu fainali ya mchujo, huku washindi wa michezo hiyo wakipangwa kukutana kwenye fainali ya Path C. Mshindi wa fainali hiyo atakwenda Qatar, na aliyeshindwa atakosa Kombe la Dunia.
Scotland na Wales zitahitaji kupita Ukraine na Austria ili kuendelea kuwa na ndoto za kutinga fainali huko Qatar, huku washindi wa michezo hiyo wakikabiliana kwenye fainali ya Path A.
“Ni droo ngumu sana kwetu,” bosi wa Italia Roberto Mancini alisema, “kwa sababu Macedonia Kaskazini ni timu nzuri na, kama tutashinda, tunapaswa kucheza ugenini dhidi ya Uturuki au Ureno katika fainali. Ni nguvu sana.”
Wiki nyingine ya kushinda mamilioni ukiwa na kasino maridhawa za meridianbettz. Mchezo pendwa wa Fai Cai Shen unakupa thamani ya dau lako, kwa kiasi kidogo cha dau unaweza kushinda mkwanja mrefu.


