Hisia za mashabiki wa soka Tanzania leo zitaelekezwa katika Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam ambako kutachezwa mechi ya watani wa jadi Simba na Yanga kuanzia saa 11 jioni ikiwa ni ya mzunguko wa kwanza wa ligi kuu msimu huu.

Timu hizo zinakutana huku Yanga wakiongoza msimamo wa ligi wakiwa na alama 19 na Simba ipo nafasi ya pili ikiwa imekusanya jumla ya alama 17 huku kila timu ikiwa imeshacheza mechi saba.
Mara ya mwisho kukutana Yanga iliibuka na ushindi 1-0 mchezo wa Ligi kuu hivyo mchezo wa leo haitakuwa rahisi kupoteza tena.
Kikosi cha Yanga Kinachoweza Kuanza: Djigui Diarra, Djuma Shaban, Shomari Kibwana, Dickson Job, Bakari Nondo, Mwamnyeto Yannic, Bangala Khalid, Aucho Jesus, Ducapel Moloko, Feisal Salum, Abdallah Fiston, Kalala Mayele, Saido Ntibazonkiza ” Antibiotic “
Kikosi cha Simba kinachoweza kuanza: Aishi Manula, Israel Patrick Mwenda Mohammed Hussein Zimbwe Pascal Wawa Hennock Inonga Baka Jonas Mkude Benard Morrison Sadio Kanoute Meddie Kagere Rally Bwalyam Hassan Dilunga
NB; Vikosi kamili vitatangazwa saa moja kabla ya mechi kuanza.
Unaweza kujishindia mamilioni katika kasino yako pendwa ya meridianbettz, mchezo wa Agent Jane Blonde Return ni moja ya michezo inayopendwa kwasasa huku ikiwafanya wachezaji kuwa mamilionea kila siku. Unasubiri nini! ungana na Agent Jane Blonde akufanye milionea.
CHEZA HAPA


