Wolfsburg wameondolewa kwenye DFB-Pokal baada ya kuzidisha kubadili wachezaji wakati wa mchezo wao na Preussen Muenster wa daraja la nne katika raundi ya kwanza ya mashindano.

Timu ya Mark van Bommel iliruhusiwa mabadiliko matano, lakini badala yake walifanya sita, huku mwamuzi wa mchezo akishindwa kutambua walitumia mchezaji wa ziada katika mchezo ambao walishinda 3-1.
Hii sio mara ya kwanza kwa korti ya michezo kuwaondoa Wolfsburg kutoka DFB-Pokal, kwani walitupwa pia nje ya mashindano mwaka 2004 baada ya kumchezesha Marian Hristov, ambaye alikuwa amesimamishwa kutoka kwenye klabu yake ya zamani, Kaiserslautern.

Hiyo ni sawa na ile iliyotokea kwa Real Madrid katika Copa del Rey mwaka 2015/16, wakati walimtumia Denis Cherishev licha ya yeye kutostahili kuchaguliwa baada ya kukusanya kadi tatu za njano katika toleo lililopita.
Ni muda wa kuwa milionea na kasino za mtandaoni za meridianbet, mchezo wa Sahara Riches unakupa nafasi ya kushinda mkwanja mrefu. Matajiri wa jangwani wanataka wakupe mkwanja leo.



Issa
Pole yao
Sarah
Pole yao
Sania+mapua
Hii noma