Martin Braithwaite amekanusha vikali madai ya kwamba tayari ameomba jezi namba 10 inayomilikiwa na fundi wa mpira Lionel Messi.
Taarifa za Spain zinadai Braithwaite amekuwa na matarajio ya kuichukua namba ya mchezaji huyo wa historia katika klabu ya Barcelona na yupo kwenye mazungumzo na the Blaugrana.
Messi ameitaarifu Barca shauku yake ya kuataka kuondoka Camp Nou huku akihusishwa kutua katika klabu ya Manchester City na kuwashangaza watu wengi kuhusu maamuzi yake ya kutaka kondoka katika klabu aliyodumu nayo kwa miaka mingi.
Lakini, Braithwaite amesisitiza hajafanya kitu kama hicho na amsema huko ni kukosa heshima.

“Watu wanafikiria nini? “kiukweli sijaenda katika klabu na kuomba namba ya Messi,” aliiambia Danish newspaper BT “itakuwa ni ukosefu wa heshima.
“Nahisi kwamba watu wanao kuja na aina hizi za stori hawana heshima hata kwa watu wengi.
“Mambo mengi yameandikwa kuhusu Messi na sijui nini kimetokea. Naweza kusema Messi ni mchezaji mkubwa na mchezaji mwenzangu katika timu ya Barcelona.
“Ni mchezaji bora wa muda wote, amefanya mambo makubwa katika klabu na kama akiondoka klabu itakuwa imepoteza mtu muhimu sana.
Braithwaite alisaini mkataba na Barcelona mwezi Februari akitokea klabu ya Leganes, kandarasi yake itaacha kufanya kazi mwaka 2014.
“Nina mkataba wa miaka minne zaidi na Barcelona, nina muda mwingi kucheza hapa ninafuraha.
SHINDA NA HI LO
Sasa hii ni rahisi zaidi kupata USHINDI! Unatabiri karata ipi ipo chini au juu, kisha unakusanya mkwanja wako.


Sadick
Endapo Messi ataondoka Barcelona nahisi jezi namba 10 itapumuzishwa kwa heshima yake kwa sababu ya mchango wake mkubwa kwa klabu hii ya Catalonia#meridianbettz
Povel
Jezi namb 10 inabid waipumzishe kwa muda kwan kwa Barcelona ya sasa cjaona mtu wakumpa jezi hyo mpka pale watakavyo jilizisha au mpka hatakapo patikana mtu mwenye uwezo wa kukaribiah Messi legendary
Shafii
Jezi namba 10 ni jezi ya mafundi endapo messi atachomoka barca sidhani Kama wanaweza wakamkabizi mtu mwengine kiheshima zaidi kwa wakati huu.
Issa
Ni namba ya heshima pale kwaio mtu atakaekabidhiwa itabidi awe na vitu adimu kama vya leo mess
rama
kwel kabisa uwezi vaa viatu vya messi
Rehema
Asante kwa taarifa
Sabrina
Huu ni uzushi ndio maana kakanusha mambo ya uvumi hayausiani na yeye
Rose kapinga
Inabidi apewe mtu ambaye atakua na maajabu kama ya messi,vinginevyo ikae kabatini tuu!!!
Hope mwaikuka
Hyo mamba sio saiz yako
Khadija
jamani kwanini aombe namba10 ya messi kwani s achukue namba nyengine
Samira
Atafute namba yake atoke kivyake asitafute kutokea kupitia messi
aisha
Braithwaite unakwama wapi mbona unahofia au uwezo wa kuvaa kiatu cha messi huna😆😆😆😆😆😆😆😆😆😆😆
Amiri Kayera
Habar za kumchafua Kwa mashabik
Theckla
Tutasikia mengi kwa kweli
Ester jackson
Kuvaa jezi na namba kumi sio tatizo tunataka kujua anauwezo wa kuitumia au mtataka umaarufu kupitia mamba hiyo
Saupha mohamed
Awwzi kuvaa viatu vya messi mwacheni mesii aitwe messi
Sauda
Namba 10 inabidi apewe fundi kama Messi..
magdalena
hii namba kumi wangeiweka tu kwanza pembeni mpaka watakapompata mtu fundi kama messi
Tatu
Braithwaite anataka kusafilia nyota ya mess
felister
ahsante Braithwaiteb kwa kutujuza mana uvumi umezidi
Dorophina
Jezi namba 10 sidhani kama Kuna mtu ataimiliki itakaa kama kumbukizi ya Messi kwa mchango wake ndani ya barca
Caroline
Binadamu kuongea ni kawaida
Zeiyana
Hatakama akichukua hiyo no hawezi kulingana na uwezo alio kua nao ukiangalia messi alikua mfalume pale Barcelona
Aziza mushi
Duh kweli tutazidi kuskia mengi
Ernest
Jezi namba kumi itawekwa makumbusho huko Catalonia na haitokuja kuvaliwa tena ndani ya Barca, Hakuna na hatotokea wa Kupewa.
David Pere
Jezi namb 10 inabid waipumzishe kwa muda kwan kwa Barcelona ya sasa cjaona mtu wakumpa jezi hyo mpka pale watakavyo jilizisha au mpka hatakapo patikana mtu mwenye uwezo wa kukaribiah Messi
Lydia Emmanuel Magoti
Jezi ya namba 10 nijezi yakiwango chake Sasa yeye anakiwango Kama Cha Messi au anataka nyota ya Messi atasubili Sana kwa Jezi ya Messi
Salma ngende
Anatamani sana awez sema ukweli
Neema
Bora kaongea ukweliii
Agness
Ni sawa anachosema Ni sahihi
Furahav
Mmmh noma sana.
Nasra
Namba kumi Ni ya heshima atafutwe mrithi atakae itendea haki camp no.
Hidaya
Jamani messi sio kufananisha na mtu mwingine
Shani
Namba 10inabid ipate mtu makini pale barca
Latifa juma mohamed
Ni mchezaji bora wa muda wote, “MESSI” amefanya mambo makubwa katika klabu na kama akiondoka klabu itakuwa imepoteza mtu muhimu sana, na kwa mchezaji braithwaite ajue kwamb ht Kama akivaa jezi no: haiwezi kufikia kiwango cha Messi.
Genia Sikaluzwe
Duuuuh noma
Fatina mfigi
Mmmh!
Gabriel
Jez no 10 itulie Kwanza muda kwan kwa Barcelona ya sasa cjaona mtu wakumpa jezi hyo mpka pale watakavyo jilizisha au mpka hatakapo patikana mtu mwenye uwezo wa kukaribiah Messi
Samiah
Mmh
Mwanahamisi
Bora kaongea ukweli
farida ahmadi
Du itakuwa kalii kuvaa jezi ya Messi
warda
habari nzuri