Roberto Firmino amekanusha kwamba yupo kwenye vita binafsi na Diogo Jota kwa kuigombea namba tisa katika timu ya Liverpool.
Jota yupo kwenye fomu tangu atue akitokea Wolves kwa kitita kinachoripotiwa £41m na amekuwa na mataokeo makubwa chanya kwa Jurgen Klopp.
Mchezaji huyo mwenye umri wa 23 amefunga magoli matatu katika michezo sita ndani ya Premier League na kufunga magoli manne katika mechi tatu za Champions League ikijumuishwa na hat-trick katika ushindi wa 5-0 dhidi ya Atalanta.
Although ingawa amecheza mechi chache katika ligi kuliko Firmino msimu huu, Jota amejaribu kupiga mashuti 13 kama Firmino ambaye amefunga goli moja pekee.
Kwa kiwango hicho Jota amembadili nafasi Firmino katika festi ileveni lakini amesisitiza wala hashindani na Jota katika nafasi hiyo.
“Liverpool ina kikosi cha wachezaji wakubwa, kwa hiyo kupata nafasi hapa siyo rahisi na nilitumika katika nafasi hiyo.” Firmino alisema kuelekea mchezo wa Jumapili dhidi ya Leicester City hii ni kwa mujibu wa Mirror.
“Diogo ni mchezaji bora kabisa na anapata ushirikiano mzuri kwenye kikosi, wote tunacheza kwa bidii kisha kocha anachagua nani ataanza nani atacheza nani atakua nje, sina vita yoyote binafsi na yeye.
Hauhitaji kuwaza linapokuja suala la ubashiri na odds kubwa. Bashiri na Meridianbet ukiwa popote ufurahie ushindi mkubwa katika michezo mbalimbali na hadi milioni 16 kwenye michezo ya kasino.



Sania
Kwahiyo ni uzushi tu
Sadick
Usajiri wa Diogo Jota ulikuwa makini na Firmino bado ana kiwango kuzuri,ni kawaida mchezaji mpya anayejitambua anaposajiriwa na timu kubwa hujituma zaidi kuchukua nafasi za waliokuwepo
Lydia Emmanuel Magoti
Firmino bado ana kiwango kizuri Sana namchezaji akisajiriwa kwenye krabu lazima apambane awe kwenye nafasi nzuri
Hopemwaikuka
Kila mtu yuko na umuhimu kwenye kiwango chake achen kuwashndanisha
Angelina
Firmino yuko vizuri sana
Caroline
Firmino ana kiwango kizuri Sana
ester jackson
Asante kwa taarifa
Sauda
Firmino anajitahidi
Adelta
Sio poa
Elika
Kijana yuko makini
Fatuma kasomo
Asante kwa taarifa meridianbet
aisha
Kijana machachali namkubali sana
samiah
Namkubali sanaa kjn
Nasra
Asantee kwa taarifa
Rehema
Sio poa
Povel
Nice update
Asia Abdy
Firminho ni mchezaji mzuri sana
Janeflora malisa
Si sawa
Saupha mohamed
Jamaa yupo vizuri
Theonestina
Duuuh
Mwajumah
Firmino Yuko vizuri sana
Fatina mfingi
Mmmh
Tatu
Firmino yupo vizuri
magdalena
duh hii ni balaa sana kwa watu wawili kulilia namba moja
Mariam mtandama
Duuuh
Sania
Yupo vizuri huyo kijana
Issa
Diogo jota mtu mwingine firmino ajafika le vo zake anfunga si kwa klabu hata spain
warda
Watu kwa kuzushia wenzao