NYOTA wa Mbao, Nasri Daudi tayari ametua nchini Hispania kwa ajili ya kufanya majaribio huku akieleza kuwa mipango yake ni kubakia huko.
Nasri anakumbukwa zaidi baada ya kufunga bao pekee kwenye mchezo wa michuano ya Shirikisho la Azam dhidi ya DTB (Singida Big Stars) na kuipeleka timu yake kwenye hatua iliyofuata.

Akizungumza baada ya kuwasili nchini humo, Nasri amesema kuwa “Namshukuru Mungu nimefika salama hapa Hispania ninachosubiri kwa sasa ni utaratibu.

“Ninawaomba watanzania waweze kuniombea nifanye vizuri kwenye majaribio yangu kwani mipango yangu ni kuhakikisha nafanya vizuri ili niendelee kubaki huku na kucheza soka.”


