Klabu ya Real Madrid leo imehitaji majibu na maelezo kwa kile kilichotokea kwenye mchezo wa fainali ya ligi mabingwa ulaya usiku wa tarehe 28 may 2022 ambapo klabu hiyo ilikutana na liverpool na mchezo ulichelewa kuanza kwa dakika 35 kutokana na fujo.
Mashabiki wa klabu zote mbili walikumbwa na kadhia ya kupigwa mabomu ya machozi na kupigwa na polisi wa Ufaransa na fujo hizo zilipelekea mchezo huo kutokuanza kwa wakati na kuleta taharuki duniani.

Real Madrid wamejiunga na wakosoaji wengine kutokana na mamlaka za nchi hiyo kushindwa kuweza kuzuia vurugu zisitokee kwenye mchezo huo wa fainali.
“Tunataka majibu na maelezo ambayo yataeleza ni nani anayewajibika kwa kuwaacha mashabiki bila msaada na ulinzi. Baadhi ya wafwatiliaji kwa ujumla walikuwa na tabia nzuri muda wote.
“Wafwatiliaji na mashabiki wetu wanastahili majibu na anayepaswa kuwajibika awajibike ili tukio kama hili lisije kutokea kwenye mpira wa miguu tena.”
SHINDA Samsung A32 ukiwa na mchezo wa Aviator kwenye Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet! Kwea pipa ukusanye zawadi zako pamoja na ushindi mnono wa mkwanja!


