Barbara:Mgunda Hana Baya Kafuata Maelekezo

MTENDAJI Mkuu wa Simba SC Barbara Gonzalez alisema kuwa kwa mara ya kwaza timu hiyo baada ya kipindi kirefu kupita imeongozwa na makocha Watanzania kwenye mchezo wa kimataifa na kufanikiwa kupata ushindi.

Barbara:Mgunda Hana Baya Kafuata Maelekezo

Barbara alisema alichokifanya kocha Juma Mgunda na Seleman Matola wikiendi iliyopita ni kufuata maelekezo ya uongozi na kutimiza yale yote ambayo walikubaliana wayafanye akiwa katikati ya uwanja na yameonekana.

Barbara:Mgunda Hana Baya Kafuata Maelekezo

Barbara alidokeza kuwa: “Tumefurahia kuanza na ushindi tukiwa ugenini na kwa mara ya kwanza Simba SC ikiongozwa na makocha wazawa kwenye mechi kubwa ya kimataifa.

“Walichokifanya ni kutimiza makubaliano yetu na Mgunda anajua nini sisi tunahitaji na wapi tunatakiwa kufika kwenye mashindano hayo. Jambo zuri tumeona alichofanya uwanjani.

“Naamini kuwa atafika kule tunakohitaji kuanzia kwenye hatua ya makundi, robo fainali na kuvuka hadi kwenda fainali kama ambavyo kila mwanasimba anahitaji.”.Mtendaji Mkuu wa Simba.

Barbara:Mgunda Hana Baya Kafuata Maelekezo

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.