Pan African Kuifuata Copco Kesho

Kikosi cha Pan African kesho jumatano kinatarajia kuondoka kuelekea Mwanza kwa ajili ya mchezo wao dhidi ya Copco.

Pan inayonolewa na Kocha Mkuu, Iddy Cheche kinacheza mchezo huo wakiwa na kumbukumbu ya kupata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Fountain Gate.

Ofisa Habari wa Pan African, Leen Essau amesema: “Kikosi chetu kipo vizuri na tayari leo jumanne kimeanza mazoezi ya kujiandaa na mchezo wa ligi.

“Kuna mchezaji ambaye ni Ayoub Mohamed alikuwa majeruhi tayari ameanza mazoezi na hivi karibuni ataonekana tena kwenye kikosi.

“Timu itaondoka Dar kesho jumatano ili alhamis wafike Mwanza na kupumzika, Ijumaa watafanya mazoezi mepesi tayari kwa mchezo wa jumamosi.”

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.