Simba Kujiuliza Mbele ya Horoya Hii Leo

Klabu ya Simba inatarajia kushuka dimbani leo kwa Mkapa kukiwasha dhidi ya Horoya kwenye mchezo wao wa ligi ya Mabingwa barani Afrika huku kila timu ikihitaji kufuzu hatua ya robo fainali.

 

Simba Kujiuliza Mbele ya Horoya Hii Leo

Mchezo huo utapigwa majira ya saa 1:00 usiku hii leo katika dimba la Benjamin Mkapa ambapo ni pointi tatu tu ambazo zitagombaniwa leo. ODDS KUBWA unazipata ndani ya Meridianbet.

Simba kwenye mchezo wa kwanza walipokutana, alipoteza kwa bao 1-0 ugenini na hii leo amekuja na kaulimbiu inayosema kuwa “Tunaitaka Fainali” ambayo amekuja nayo Afisa habari wa klabu hiyo Ahmed Ally.

Kaulimbiu hiyo ni kwaajili ya kuhamasisha wachezaji kucheza kwa ari lakini pia mashabiki kujaa uwanjani kwaajili ya kuitazama timu yao inafanya vizuri na kupata matokeo yatakayowawezesha kwenda hatua inayofuata.

Simba Kujiuliza Mbele ya Horoya Hii Leo

Horoya inashikilia nafasi ya tatu wakati mnyama yeye anashikilia nafasi ya pili hivyo kutokana na msimamo jinsi ulivyo kila timu kama ikipata matokeo kwenye mechi mbili zizlizobaki inaweza kwenda robo fainali.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.