Aubameyang amkosha Didier Drogba kutokana na uamuzi wake wa kuamua kuondoka FC Barcelona na kujiunga Chelsea.

Nahodha huyo wa zamani wa Arsenal, aliachwa na Barcelona miezi sita tu baada ya kuondoka Arsenal kutokana na hali mbaya ya kutofautiana kwake na Mikel Arteta.
Kuwasili kwa Robert Lewandowski, pamoja na hali mbaya ya kifedha ya Barcelona, ilimlazimu mchezaji huyo kutopewa nafasi na hivyo uhamisho wake wa Chelsea uliotarajiwa ulikamilika siku ya mwisho.

Nyota huyo ataungana tena na kocha wake wa zamani wa Borussia Dortmund Thomas Tuchel, ambaye hitaji lake la mshambuliaji mpya wa kati limechagizwa na vipigo vya hivi karibuni dhidi ya Leeds na Southampton.

Drogba Aliandika kwenye Twitter: “Hatimaye!!!!! Kumbuka wakati tulizungumza kuhusu hili miaka iliyopita Nimefurahi.”

Staa huyo huenda akaingia moja kwa moja kwenye kikosi cha Chelsea, kabla ya mchezo wa Jumamosi dhidi ya West Ham Uwanja wa Stamford Bridge na mchezaji huyo wa kimataifa wa Gabon anatazamiwa kucheza.

Aubameyang Alisema: ‘Nina furaha sana.
“Ni heshima kuwa sehemu ya timu hii na siwezi kusubiri kuanza. Nina jukumu ambalo halijakamilika kwenye Ligi Kuu kwa hivyo ni vizuri kurejea tena.”

