Chozi la Suarez kwa Barcelona

Inaendelea..
Lazima ndani ya Barcelona kuna umoja, ukaribu na urafiki. Lakini aina ya mashabiki ambao Suarez atawakumbuka na mazoea kama mwanadamu wa kawaida, hivyo ni lazima kumwaga chozi. Yote sawa, lakini kama utabahatika kusoma kitabu chake hicho utagundua mapenzi yake na Barcelona hayakuanza wakati anakwenda kujiunga nayo lakini Barcelona imo ndani ya maisha yake kupitia Sofi.
Suarez hakupenda shule, ukizingatia familia yake ilikuwa ni ya kimasikini sana, hawakuwa na muda wa kuifuatilia sana mienendo yake shuleni. Lakini Sofi alipinga mara zote na kumhimiza kusoma. Muda mwingi, Suarez alilazimika kuazima nauli asafiri zaidi ya kilomita 30 kwenda kumtembelea Sofi nyumbani kwao. Baadaye familia ya Sofi ilihamia Ulaya, ilihamia jijini Barcelona mwaka 2003 na huu ndio ulikuwa mwanzo wa Suarez kutamani kwenda kucheza barani Ulaya kwa kuwa alitaka tena kuungana na Sofi ambaye alimuona ndiye tegemeo katika kila kitu kwake. Mara moja, alialikwa Ulaya na Sofi na bado anavyokumbuka walivyoibia kwenda kupiga picha ndani ya Uwanja wa Camp Nou kwa kuwa hawakuwa na fedha za kulipia zoezi la kutembelea uwanja huo. Unaona namna maisha yalivyokuwa na baada ya kurejea Uruguay, aliamua kufanya juhudi kuu, akapambana hadi alipofanikiwa kusajiliwa na klabu ndogo ya Groningen ya nchini Uholanzi, hii ilikuwa ni mwaka 2006.
 Suarez aliongeza juhudi akijua alistahili maisha bora kwa kuwa Ulaya ni mapambano zaidi na mara nyingi alitaka kumridhisha Sofi kwa kuwa alijua alivyompigania na yeye hakuwa na elimu wala hakuwahi kufaulu, hivyo alipambana akijua mkombozi ni mpira. Alifanikiwa kujiunga na Ajax mwaka 2007, mwaka 2011 akatua Liverpool na 2014 ikawa ni Barcelona lakini kumbuka mwaka 2013 alitaka kujiunga na Arsenal lakini Steven Gerrard wakati huo akiwa nahodha wa Liverpool, alimzuia na kumueleza acheze msimu mmoja akiwa Anfield na huenda akajiunga na Real Madrid, Bayern Munich au FC Barcelona na si Arsenal tena, na kweli msimu uliofuata, hilo likatokea.
Unaona kiasi gani Mji wa Barcelona ulivyokuwa sehemu ya kumvuta Suarez kwenda Ulaya, kwa kuwa ulikuwa mji wake wa kwanza kukanyaga akiwa Ulaya lakini mapenzi yake na Barcelona, yalimfanya asichoke sababu alitamani siku moja ataichezea. Bila shaka ilikuwa ni klabu yake pendwa ambayo alifanikiwa kuifikia. Sofi, anabaki kuwa shujaa wake kwa kuwa unaona alivyoshiriki katika maisha yake wakiwa watoto kutoka katika familia zenye aina tofauti kabisa. Kwani baba mzazi wa Sofi alikuwa bosi wa benki na walihama baada ya benki kufungwa kutokana na anguko la kiuchumi mwanzoni mwa miaka ya 2000.

Chozi la Suarez si kuondoka tu FC Barcelona, linajumuisha mengi na “undugu” wa historia ya maisha yake na Jiji la Barcelona, unamfanya akumbuke mengi aliyopitia akijua sasa anahamia katika jiji pinzani la jiji lake kipenzi, timu yake kipenzi lakini maisha, hayakupi nafasi ya kuchagua kila unachokitaka kama leo Suarez ni tajiri, maisha yake ni ya kifahari kwa kuwa mshahara wake kwa mwaka utakuwa zaidi ya pauni milioni 6 (zaidi ya Sh bilioni 17), lakini hana ujanja, lazima aondoke Barcelona kwa maana ya klabu na jiji pia.


Beti kwa Kitochi Kushinda 300,000,000!

Unajua kuwa unaweza kushinda milioni mia tatu kwa buku tu? Ndiyo! Unaweza kushinda kwa kupiga *149*10# na kubashiri. Ingia mchezoni!

Soma Zaidi

31 Komentara

    Suarez alikua mtu muhim barca sema kocha hakuwa na mahesabu nae lakin ni fowad makin na hilo amelionyesha mechi ya kwanza atletico kwa kupiga goli 2

    Jibu

    Duh kumbe Suarez aliipenda barca kwa sababu ya historia yake na jiji la Barcelona pamoja na kumfata sofi nashukuru kwa kunijuza

    Jibu

    Suarez ni mchezaji makini sana barca imepoteza kumuacha huyu

    Jibu

    Striker Bola kuwah kutokea alikiwasha San alivokua Liverpool

    Jibu

    Asante kwa taarifa

    Jibu

    dah barca wamemkatili sana Suarez

    Jibu

    Kocha nazani hakumpenda tu Suarez ila ni mchezaji mzuri sana

    Jibu

    suarez apige moyo konde asonge mbele kocha wa barca alishamkataa kitambo tu

    Jibu

    Dah Suarez piga moyo konde

    Jibu

    Suarez maisha popote angalia ndoto zako zitimiye

    Jibu

    Suarez alikuwa na mapenzi ya dhati na timu yake alitamani kuitumikia mpaka mwisho

    Jibu

    Suarezi kikubwa maslahi tu popote kambi

    Jibu

    Barca awamefanya makosa sana kumuacha suarez kwan ni mchezaji mzuri sana

    Jibu

    Suarez ana mchango mkubwa sana Barcelona

    Jibu

    Baadae Barcelona watakuja kajuta kumpoteza

    Jibu

    Suarez akutaka kuondoka kabisa Barcelona sababu alikuwa na mapenzi nayo kutoka moyoni tatizo kocha akupendeza abakie pale

    Jibu

    Duu kweli Suarez Barcelona kwenye moyo wake inamchango mkubwa ndomana lazima angiwe nasimbazi Sana kundoka hapo kwenye krabu ya Barcelona ila mzeebaba usikate tamaa kokote kambi utapata ukitakacho Suarez piga kaz

    Jibu

    What a touching story!!! Suarez lives already on his dream now its a time to wish and dream for the new things

    Jibu

    Kumbe aliipenda timu yake. Duu maisha popote usijal

    Jibu

    Dah! Hii aikuwa sahihi

    Jibu

    Popote kambi cha msingi akaze tuu

    Jibu

    Kwani kambi popote

    Jibu

    Suarez kiboko

    Jibu

    Suarez yupo vizurii

    Jibu

    Suarez kikubwa maslai

    Jibu

    Suarez alikua mtu muhim barca sema kocha hakuwa na mahesabu nae lakin ni fowad makin na hilo amelionyesha mechi ya kwanza atletico kwa kupiga goli 2

    Jibu

    Barca wamemfanyia vibaya Suarez

    Jibu

    Kila LA heri hata hapo

    Jibu

    Suarez dunia mApito wanadamu soon watu wakuwah min ni vigeu geu sana

    Jibu

    kocha hakuwa na mahesabu nae lakin ni fowad makin

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.