Cristiano Ronaldo Kuchagua Meneja Mpya Juve

Suala la nani atakuwa meneja anayefuata klabuni Juventus limekuwa likigonga vichwa vya habari zaidi siku za hapa karibuni. Ripoti zinamtaja nyota wa klabu hii Cristiano Ronaldo kuchagua meneja anayependa awa meneja mpya wa klabu hiyo.

Juventus wanatarajia kuachana na Massimiliano Allegri ambaye ameamua kuondoka klabuni hapo baada ya mafanikio ya miaka kadhaa. Swali kubwa ni nani ataichukua nafasi yake.

Ripoti zimekuwa zikimuhusisha aliyekuwa meneja wa Manchester United Jose Mourinho na kibarua cha umeneja klabuni hapo. Hata hivyo Carlo Ancelotti pia anatawa kuwa ni moja ya tamanio la klabu hii kuziba pengo la Allegri.

Kwa mujibu wa chapisho la Express, Ronaldo angependelea zaidi Ancelotti kuwa meneja wa klabu hiyo dhidi ya Jose Mourinho. Ronaldo anawafahamu vyema wawili hawa, ana mchukulia Mourinho kama shujaa mkubwa wa soka licha ya kutimuliwa hivi karibuni Chelsea pia Man United.

Hata hivyo, Cristiano Ronaldo hataepuka kucheza chini ya meneja mpya msimu ujao na kwa namna yeyote ile atakubaliana na meneja yeyote atakayekuja klabuni hapo.

Makala ijayo

4 Komentara

    Habari njema#meridianbettz

    Jibu

    Nzuri sana

    Jibu

    Habar njema

    Jibu

    Waoooooo kazi nzuri

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.