Baada ya matokeo ya vipimo vya COVID19 kuonesha kuwa hali sio shwari nchini Uingereza, uongozi wa EPL umesema hauna mpango wa kusitisha michezo inayoendelea msimu huu.
Kumekuwa na hali ya sintofahamu kuhusu muendelezo wa michezo ya EPL baada ya vilabu mbalimbali kuathirika na COVID19, michezo kadhaa ilighairishwa na baadhi ya vilabu kuzuiliwa kuingiza mashabiki viwanjani.
Kutokana na sintofahamu hiyo, Premier League imetoa tamko kuwa “hatujajadili kusimamisha msimu.
“Ligi itaendelea kuzingatia utaratibu wa kujilinda na COVID19 ili kuwezesha michezo kuendelea kama ilivyopangwa, taratibu hizi zinaendelea kusimamiwa na serikali.
“Kwa kuzingatia usalama wa wachezaji na wafanyakazi wote kwenye vilabu, ligi inaungana na vilabu katika kutekeleza taratibu zilizowekwa.”
Licha ya kwamba EPL itaendelea, mashabiki hawatoruhusiwa tena kuingia viwanjani kama sehemu ya kujilinda na COVID19. Ni Liverpool na Everton pekee ndio vilabu vilivyokuwa vinaweza kupokea mashabiki 2,000 na sasa vilabu hivyo havitoruhusiwa kufanya hivyo tena.
VUNA SHEA YAKO YA 230,000,000TSH NA UFURAHIE MSIMU HUU WA SIKUKUU!!!
Kupitia Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet, jiwekee nafasi ya kupata shea yako ya 230,000,000Tsh kupitia mchezo wa Secret Santa. Hakika hutojutia kufurahia msimu huu wa sikukuu ukiwa katika nyumba ya mabingwa ya Meridiabet. Unasubiri nini?



Sania
Corona ituache jamani
Shakila mrope
Du corona ni janga kubwa
Rahmal
Dar colona sio poa
Adelta
Coronavirus sio poa
Neema juma
Maamuzi waliyosema ni sahihii kabisa
Sabrina
Ni sawa ila wachukue tahadhari
Fatina mfingi
Tahadhari muhimu
Ernest Kimeru
Hii ni hatari sana lakini Corona imeshaonyesha kuwa ni ugonjwa ambao tunatakiwa kuishi nao
Caroline
Wachukue tahadhari
warda
Safi sana nimependa msimamo wao
Dorophina
Habari njema ila tahadhari ni muhimu maana corona haiwezi kuisha leo
Angelina
Corona inazidi kuwa kikwazo jamn
Tatu
Corona sio poa
Janeflora malisa
Corona ttz
Sarah
Corona noma sana
Hopemwaikuka
Bora tu
Issa
Covid inaleta hasara
Chiku
Hawaja chelew tahadhari muhim