Kieran Trippier Kufunguwa Kujihusisha Na Soka

Kieran Trippier Afungiwa kutojihusisha na Masuala ya Mpira wa Miguu Baada ya kuvunja Sheria za FA kufuatia kujihusisha na Masuala ya Ubashiri (Betting). Beki huyo wa zamani wa Tottenham anayekipiga Atletico Madrid amefungiwa kujihusisha na shughuli za mpira kwa kukutwa na makosa ya kuvunja sheria za michezo kwa kubashiri.

Kwa mujibu wa Taarifa ya FA, Trippier amekutana na kifungo hicho kwa kukutwa na kosa la kuvujisha habari ya ndani kuhusu uhamisho wake kutoka Tottenham kwenda Atletico Julai 2019, ambapo habari hizo zilitumika kufanyiwa ubashiri juu ya uhamisho wa mchezaji huyo.

Trippier amepewa hadi kufikia Mei 18 kuwa amekata rufaa, nyota huyo wa kimataifa wa England mwenye umri wa miaka 29 sasa anacheza mpira wake nchini Uhispania, hivyo FA italazimika kuomba FIFA kutekeleza kifungo hicho cha kutojihusisha na maswala ya soka. Trippier inaripotiwa kuwa amekiuka sheria mbili kama zile za mchezaji wa zamani wa Chelsea na Liverpool Daniel Sturridge. Ikumbukwe Sturridge alifungiwa miezi minne na alipigwa faini ya Pauni 150,000.

8 Komentara

    Spurs miss him at Right Back #MeridianbetTZ

    Jibu

    Mmh hatorudia kubashiri.

    Jibu

    Ndo pole kwake

    Jibu

    Bora apewe adhabu iwe funzo kwa wachezaji wengine

    Jibu

    Akishajua kosa lake hatorudia tena

    Jibu

    Yupo poa sanaa

    Jibu

    Kwel wezetu sheria zao nzur

    Jibu

    kafungiwa kwa muda gani…?

    Jibu

Acha ujumbe