Bosi wa Realo Madid Zinedine Zidane amekuwa akihusishwa sana na nyota wa Real Madrid Eden Hazard. Staa huyu alishawahi kuweka wazi kuwa Real Madrid ni klabu ya ndoto zake toka alipokuwa mdogo huku akionesha matamanio yake ya kufundishwa na meneja Zidane ambaye ameweka wazi pia kuwa nyota huyu alimkosha wakati wote.
Zinedine Zidane, anaweka wazi pia kwa upande wake amekuwa akimkubali nyota huyu kwa mda mrefu, amekuwa akimfikiria mara zote akiona kama ni mmoja wa wachezaji bomba zaidi.
Hazard alitarajiwa kuwa angesepa Chelsea, na mapema mwezi wa pili alisema kuwa tayari alishafanya maamuzi juu ya hatma yake klabuni hapo. Zidane anasema mara zote amekuwa akimkubali na amekuwa akimuona mara nyingi sana toka alipokuwa anachezea Ufaransa.
Kwa mujibu wa jarida moja la Uingereza, London Evening Standard Hazard, ambaye mkataba wake klabuni chelsea unafika tamati mwaka 2020 anatarajia kusepea Hispania msimu huu wa joto. Kama mara zote Hazard alimkosha Zidane, bila shaka meneja huyu atanyoka naye kumshusha Real Madrid.

