Van de Beek."Muda Wangu Utafika Man United"

Donny Van de Beek, Muholanzi asiye na maneno mengi ila uwezo wake uwanjani ni uthibitisho wa kiwango safi cha kucheza soka. Baada ya kutua Man United, mambo yamebadilika kidogo.

Man United ilimsajili Van de Beek katika dirisha la majira ya kiangazi kwa dau la pauni milioni 40 akitokea Ajax alipoanzia maisha yake ya soka na kujitengenezea jina kubwa kwenye ulimwengu wa soka.

Akiwa United, Donny amecheza michezo michache akianzia benchi kwenye michezo mingi ya EPL. Licha ya kutopata nafasi nyingi za kuonesha kipaji chake akiwa United, nafasi chache alizopata alizitumia vyema kuonesha yeye ni mchezaji wa aina gani.

Wachambuzi na wapenzi wa soka maeneo mbalimbali duniani wamekuwa wakimtupia maneno kocha wa Man United – Ole Gunnar Solskjaer kwa kushindwa kumtumia vizuri mchezaji huyu licha ya kuwa na kiwango kikubwa kuwazidi wachezaji wanaotumika sana.

Solskjaer alishasema “Donny atakuwa na jukumu kubwa ndani ya United na muda wake utafika.” Kauli ya Ole inaungwa mkono na Van de Beek ambaye amekiri ni suala la muda tu na anaimani muda huo unafika ndani ya muda mchache ujao.

“Sipendi kulisema hili ila ni kweli, ningependa kupata muda zaidi wa kucheza. Ninajisikia vizuri kuwa kwenye klabu kubwa. Nilipokelewa vizuri na nilisaidiwa na kila mtu.” alijibu Donny baada ya kuulizwa na NOS kuhusu hali yake ndani ya kikosi cha Man United.

“Mimi ni mtu mwenye subira, lakini unakwenda pale ukiwa na lengo la kucheza mara kwa mara. Pia ninadhani kwa kila muda ambao nimecheza, nimeonesha ni kitu gani ninaweza kukiongeza kwenye timu.

Solskjaer amesema nini kuhusu mimi? Ninatakiwa kuwa na subira, lakini pia ninatakiwa kuendelea kufanya ninachokifanya.

“Ameona ninamchango mkubwa ninapokuwa uwanjani. Muda wangu utafika na wakati hizo fursa zinapokuja, ninatakiwa kuzitumia ipasavyo.”

Katika mechi 3 za Ligi ya Mabingwa, Van de Beek anawastani mkubwa (92%) wa kupiga pasi kuwazidi viungo wengine wa Man United – Matic (89.4%), Pogba (85.5%), Fred (84.1%), McTominay (83%) na Fernandes (73.3%).


UMEJARIBU HII POKER YA VIDEO?

Jaribu sasa hapa Meridianbet. Ukiacha ukweli kuwa itakupa burudani maridadi, bado inakuhakikishia ushindi mkubwa. Kazi kwako kukusanya ushindi!

Meridianbet Casino

INGIA MCHEZONI!

21 Komentara

    Asante kwa makala

    Jibu

    Safii Sana Van uwezo unajionyesha mpambanaji kilakitu kina kwenda namipango kajisemea Van

    Jibu

    Safi sana kijana yuko vizuri,kijana yuko makini

    Jibu

    Kijana mwenye kujituma uwanjani

    Jibu

    Kijana anajiamini sana

    Jibu

    Safi sana van uko ni kujiamini

    Jibu

    Goodnews

    Jibu

    Safi sana kijana

    Jibu

    Subira ni nzuri sana

    Jibu

    Safi Sana van umejuwa kutufurahisha
    Mashabiki

    Jibu

    Van de beek yupo vizuri sana anajua nini anafanya

    Jibu

    Nakubali van de beek

    Jibu

    vizurii

    Jibu

    Safi

    Jibu

    Good news

    Jibu

    Asante kwa makalq

    Jibu

    Muda utaongea

    Jibu

    Kila kitu kina kwenda na mda wake ukiangalia kwenye maisha ya mpira kila siku wanaibuka wachezaji wapya mwenye uwezo kupita yeye kikubwa hangalie mda wake sasa mashabiki wake wanatamani kuona uwezo wake kwa mala nyengine akiwa clabuni hapo

    Jibu

    Van de beek ni kwl wakati wakuchez united ukifikah tu

    Jibu

    Van de beek ataleta mapinduz united

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.