Juventus wanakwama kuamua hatma ya Cristiano Ronaldo, wakihitaji apunguze mshahara wake, kwa mujibu wa Sky Sport Italia.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ureno alikuwa alikuwa sehemu muhimu Jumatano katika ushindi wa 4-0 wa kirafiki dhidi ya Israeli.
Nyota huyu anahusishwa na kuondoka klabuni hapo kwa kuwa Max Allegri amerudi Turin, huku Manchester United, Real Madrid na PSG zikiwa zinaonesha nia ya huduma yake, bila kusahau Inter Miami katika MLS.
Hata hivyo, Gianluca Di Marzio anadai hakuna klabu yoyote iliyo tayari na dili la Ronaldo kulingana na mshahara mkubwa 30m ambao anapata sasa na Juventus.
Kwa hivyo, hata kwa biashara yay €30m, hakuna timu zinazoweza kumsaini CR7 msimu huu wa joto.
Chaguo pekee itakuwa kwake kupunguza mshahara wake au kusaini kandarasi ambayo itaeneza mshahara huo kwa misimu kadhaa.
Hiyo pia ni ngumu ikizingatiwa alitimiza miaka 36 mnamo Februari.
Wakala Jorge Mendes alionekana huko Milan Jumatano na alipokea ugeni kutoka wakurugenzi wa Milan, Inter na Fiorentina, lakini sio Juventus.
Chukua namba yako ya akaunti na kiasi cha pesa unachotaka kuweka, sogea kwenye duka lolote la Meridianbet lililo karibu nawe utasaidiwa kuweka pesa.
Mmmhh mbona watakuwa wamemkosea?
Kama wameshindwa kumlipa mshahara wake si waweke wazi tu
Hakuna haki hapo
Kama nihivo watakua awatendi haki
Duuh
Wamuache tu