Nyota wa Real Madrid, Luka Jovic anaripotiwa kuwa anajiandaa kulazimisha uhamisho wa kuondoka Real Madrid katika dirisha la mwezi Januari.
Tangia kuwasili kwake tokea Eintracht Frankfurt Julai 2019, staa huyu wa miaka 23 amefanikiwa kufunga magoli mawili tu kwenye mechi 39 alziocheza na Real.
Luka Jovic amepata fursa ya kucheza kwenye mechi saba msimu huu, akifikisha dakika 95 pekee uwanjani. Staa huyu aliwekwa benchi kwenye mechi ya La Liga dhidi ya Elche wikiendi iliyopita licha ya Karim Benzema kuwa nje akiuguza jeraha.

Vilabu kadhaa, wakiwepo Arsenal na Liverpool vimetajwa kuwa na nia ya kuipata huduma ya nyota huyu wa Serbia, Luka Jovic.
Kwa mujibu wa Defensa Central, staa huyu kwa sasa anafikiria zaidi kushinikiza uhamisho mwezi Januari, na atakuwa tayari kuondoka mapema tu ikiwa fursa itapatikana.
Jovic, akiwa amesalia na mkataba wa miaka minne pale Bernabeu, alitumia nusu ya msimu katika klabu ya zamani ya Frankfurt kwa mkopo.
Mkwanja umetema ndani ya kasino za meridianbettz, Mchezo maridhawa wa Aurora Beast Hunter unakupa nafasi sawa ya ushindi leo hii, kila mzunguko una nafasi ya kuibuka mshindi, na mkwanja wako unaupata kila mzunguko utakapo kamilika.


