Manchester United Kukutana na Nottingham Forest Carabao

Klabu ya Manchester United inakwenda kumenyana na klabu ya Nottingham Forest kwenye mchezo wa nusu fainali wa kombe la Carabao Cup.

Klabu ya Manchester United imefanikiwa kuting hatua ya nusu fainali baada ya kuifunga klabu ya Charlton kwa jumla ya mabao matatu kwa bila, Huku klabu ya Nottingham Forest wao wakifanikiwa kuitoa klabu ya Wolves kwa mikwaju ya penati kwenye hatua ya robo fainali.Manchester unitedManchester United imekua kwenye ukame wa makombe kwa miaka takribani miaka sita sasa huku wakitazamiwa kufanya lolote ndani ya msimu huu chini ya kocha Erik Ten Hag. Man United ilibeba taji lake la mwisho mwaka 2017 likiw taji la Europe League chini ya kocha Jose Mourinho.

Klabu hiyo ambayo imekua kwenye kiwango kizuri tangu kurudi kwa ligi baada ya michuano ya kombe la dunia wakifanikiwa kushinda michezo nane mfululizo. Klabu hiyo inaonekana inaweza kunyakua taji lake la kwanza msimu huu tangu mwaka 2017.

Manchester unitedKlabu ya Manchester United chini ya kocha Ten Hag imeanza kua timu tishio na hiyo ni kutokana na ubora ambao wamekua wakiuonesha kwa siku za hivi karibuni, Hii inawafanya kua miongoni mwa timu ambazo zinaanza kutolewa macho ndani ya Uingereza.

 

Acha ujumbe