Manuel Neuer Tuko Tayari Kuwakabili Villarreal

Golikipa na kapteni wa timu ya Bayern Munich Manuel Neuer anaimani kuwa klabu yake iko tayari kuwakabili klabu ya Villarreal kwenye mchezo wa robo fainali ya ligi ya mabingwa ulaya kwenye mchezo wao wa pili 

Manuel Neuer wakati akihojiwa alinukulia akisema, “nina furaha kwa ajiri ya mchezo wa kesho, hii ni ligi ya mabingwa, mara zote yamekuwa mashindano muhimu kwetu, tuna wachezaji wengi wadhoefu ambao wamecheza kwa muda mrefu.

Hatuna tatizo la uongozi, hilo halihitaji mjadala, tunazungumza sana na kufanya maboresho mara kwa mara, mawasiliano hapa ndio nyumbani.

Villarreal ni timu inayoshambulia vizuri sana, na kesho tutawaonyesha ubora wetu huku tukiwa na mashabiki wetu, mara nyingi tumekuwa hatuna mchezo mzuri kwenye hatua ya mtoano hasa mchezo wa kwanza kwenye klabu bingwa, tumekuwa tukipata matokeo yasiyo ridhisha, hatuogopi.”

Alipoulizwa kuhusu kocha wake Julian Nagelsmann kuhusu maandalizi ya kikosi Manuel Neuer alijibu, “Kocha amejidhatiti kwa ajiri ya mchezo, anajaribu  kutuaanda kuwa bora kadri awezavyo, hususani kwenye mbinu za mchezo.”


VUNA MKWANJA NA AVIATOR

Maana halisi ya ushindi mkubwa unaipata katika kasino ya mtandaoni ya Aviator kutoka meridianbettz. Andaa kapu la ushindi wa mkwanja na beti kibao za BUREEE.

tetesi, Tetesi za Soka Barani Ulaya., Meridianbet

SOMA ZAIDI

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.