Kocha wa Burnley – Sean Dyche amesisitiza “hana tatizo” na beki wake Tarkowski. Hii ni baada ya mchezaji huyo kusema hadharani hana mpango wa kusaini mkataba mpya.
Wiki iliyopita, Tarkowski aliweka hadharani adhma yake ya kutohitaji kusaini mkataba mpya wa kuendelea kubaki Turf Moor. Jambo hili limezua taharuki miongoni mwa mashabiki wa Burnley ikizingatiwa kwamba usajili uliopita, timu hiyo iligoma kumuachia kwa pauni 30 zilizotolewa na Leicester City.
Licha ya kucheza michezo 6 msimu huu, Tarkoswski alinukuliwa akisema “Hakuna nilichokisikia au kupatiwa ambacho pengine kitanifanya nifikirie kusaini mkataba mpya na Burnley”
Akijibu tamko hilo, Sean Dyche amesema “siku hizi wachezaji wanauwazi wa aina yake kwenye media na kulingana na maswali tofautitofauti. Aliulizwa maswali na aliyajibu kwa ukweli kama ilivyoonekana.
“Haya mambo yanatokeaga muda mwingi, sina tatizo na Tarky au mtu yeyote, ni mchezo mzuri sana kwetu, kwangu ni mchezaji mwenye kiwango kikubwa.
“Nimelisema hili kwa mwezi mzima sasa… ninashangaa kwanini hausishwi kwenye timu ya Taifa ya Uingereza, ninadhani anapaswa kupewa hiyo nafasi.
“Yale mahojiano hayabadilishi kitu chochote, zaidi anapaswa kuongeza juhudi na kufanya vizuri kwenye uchezaji wake, kwenye timu na klabu kwa ujumla. Sidhani kama hilo litabadilisha kitu chochote.”
Je, Sean Dyche atafanikiwa kumbakiza Tarkowski kwenye kikosi cha Burnley au beki huyo ataendeleza msimamo wake? Leicester City na West Ham United ni miongoni mwa timu zilizokuwa zinawania saini ya mchezaji huyo kwenye dirisha la usajili lililopita.
Hauhitaji kuwaza linapokuja suala la ubashiri na odds kubwa. Bashiri na Meridianbet ukiwa popote ufurahie ushindi mkubwa katika michezo mbalimbali na hadi milioni 16 kwenye michezo ya kasino.
Lydia Emmanuel Magoti
Duu mbona hiyo shida kugoma kusain mkataba mwingine ngoja tuone
Adelta
Tunasubiri tuone
Saupha mohamed
Dhuuu hayo mapyaa
Ester jackson
Dash Mimi naona kama kunamkanganyiko hapo mana kila mtu anajambo lake nafikiri waelewane vizuri kuhusu mkataba mambo mengine yaendelee
Caroline
Sawa tu.ashikilie msimamo wake
Sauda
Du! Ana msimamo mkali!!!
Nasra
Tunasubiri kwa hamu
magdalena
kama kaamua kutokuongeza mkataba wasimlazimishe wampe muda wa kuchagua nini anataka
Fatina mfingi
Inabid wakae chin waelewan waje na jibu moja
lombo
vzr
Rahma
Tuna subili
Samiah
Safi
Shakila mrope
Tunasubilia tuone
Hopemwaikuka
Fresh
Povel
Nice information
Sabrina
Basi sawa
Angelina
Safi
zeiyana
Tarkowiski hinatakiwa hakacheze vilabu vikubwa ili kuliendeleza soka lake
aisha
Imeisha iyoooo
Latifa juma mohamed
Safii
Rehema
Nice
Tatu
Safi
warda
Hataki kubaki sehemu moja