Sterling: Sisi Pekee Tunaweza Kujinyima Ubingwa

Raheem Sterling anadai Manchester City ndio timu pekee ambayo inaweza kujizuia kushinda Ligi ya Mabingwa wikendi hii.

Mabingwa wa Ligi ya Premia wana nia ya kuwa ba msimu wa kukumbukwa kwa kuifunga Chelsea huko Porto ili kutwaa taji kubwa zaidi barani Ulaya Jumamosi.

Chelsea waliifunga City mara mbili katika wiki sita zilizopita lakini hali ilikuwa tofauti wakati huo na Sterling anasema matokeo hayo hayana maana yoyote kwa sasa.

“Vitu pekee vinavyoweza kutuzuia ni sisi wenyewe ikiwa mimi ni mwaminifu” Raheem Sterling

Fowadi huyo wa City alisema: “Chelsea ni timu ambayo ina wachezaji wengi wenye nguvu. Tumecheza nao mara mbili na kupoteza mara mbili lakini hii ni fainali ya Ligi ya Mabingwa. Siku hiyo, mambo ni tofauti sana.”

“Vitu pekee ambavyo vinaweza kutuzuia ni sisi wenyewe ikiwa mimi ni mwaminifu. Huu ni mchezo ambao ninatarajia kibarua kigumu lakini wakati huo huo ninatarajia tupitie.”

Sterling anaweza kuwa benchi kwenye kikosi kinachoanza huko Estadio do Dragao kwani fomu ya wachezaji kama Phil Foden, Bernardo Silva na Riyad Mahrez imewafanya wapate kipaumbele katika mechi za hivi karibuni za Uropa.

Lakini pamoja na mbadala watano walioruhusiwa, kuna nafasi kubwa mchezaji huyo wa kimataifa wa England kuwa na jukumu la kucheza.

Mchezaji huyo wa miaka 26 aliondoka Liverpool kwenda City mnamo 2015 ili kuendeleza taaluma yake ya soka na anakubali kucheza mechi za aina hii imekuwa lengo lake kwa muda mrefu.


BONASI YA 50% KILA SIKU KATIKA KASINO ZA EVOPLAY HAPA MERIDIANBET.

Meridianbet na Evoplay Kasino wanakupa bonasi ya 50% ya kiasi utakachoweka katika akaunti yako leo. Unasubiri nini ni wakati wa kupiga pesa sasa na Mabingwa.

tuchel, Tuchel :Tuna Bahati Tottenham Wametusaidia Kazi., Meridianbet

SOMA ZAIDI

4 Komentara

    City wananafasi kubwa sana ya kuchukua Ubingwa wa Uefa ila kama watacheza kitimu na kuwa na nidhamu na Mchezo maana Chelsea sio timu ya kuibeza na kujitangazia ushindi mapema

    Jibu

    City kila msimu wapo vizuri

    Jibu

    Wajitume Sana maana Kila kikosi kinatamani ilo kombe

    Jibu

    City wako vizuri

    Jibu

Acha ujumbe