Klabu ya Chicago Fire imetangaza kumsajili winga wa Lyon Xherdan Shaqiri kwa mkataba wa miaka mitatu.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 30 aliondoka Liverpool na kujiunga na timu ya Ufaransa msimu wa joto, akiwa amecheza mechi 13 na mechi tatu akitokea benchi tangu uhamisho huo.
Hata hivyo, ilibainishwa Jumatano kwamba mchezaji huyo wa kimataifa wa Uswizi alihamia MLS, akiungana tena na mkurugenzi wa michezo Georg Heitz ambaye alifanya naye kazi huko Basel.

Heitz alisema: “Tunafuraha kubwa kumkaribisha rasmi Xherdan Shaqiri hapa Fire. Xherdan ni mchezaji anayebadili mchezo na mtu ambaye ataleta furaha kwa wafuasi wetu na jiji la Chicago.
“Kama mmoja wa wachezaji wa Uswizi walio bora zaidi wa kizazi chake, Xherdan anajiunga nasi katika wakati muhimu sana kwa klabu na anaamini katika kile tunacholenga kukamilisha. Tunatazamia kumkaribisha yeye na familia yake Chicago hivi karibuni.”
Chicago wamedaiwa kulipa takribani dau la £5.5m kwa Shaqiri.
Haijawahi kuwa rahisi hivi kwenye safari yako ya kuvuna mkwanja, kasino maridhawa ya meridianbettz inakuletea mchezo wa Emoticoins unaokupa nafasi ya kufanya safari yako kuwa rahisi zaidi. Wakati ni wako nafasi ni yako na Emoticoins.


