UEFA Kuwalipa Wenye Tiketi za Fainali Watu 2,700

Shirikikisho la mpira wamiguu barani Ulaya UEFA limeagizwa kuwaliapa watazamaji 2700 wenye tiketi ambao walishindwa kuangalia mchezo huo wa fainali siku ya jumammosi kati ya Liverpool na Real Madrid.

Mchezo huo wa siku ya Jumamosi ulichelewa kwa dakika 36 kwenye uwanja wa Stade de France jijini Paris, kutokana na kuwepo kwa vurugu kwenye mlango wa kuingilia mashibiki wa Liverpool na kuzuiwa mashabiki hao kutokuingia uwanjani.

UEFA
UEFA

Baadhi ya mashabiki walipuliziwa maji ya kuwasha na kupigwa na mobomu ya machozi na polisi wa Ufaransa, waliokuwa wanazuia vurugu, huku wangine wakijaaribu kupanda viunzi ili kuweza kuingia ndani.

Lakini mashabiki wengi hatimaye waliweza kuingia ndani baada ya mchezo kuanza huku wengine wakishindwa kabisa.

“Tumewaomba UEFA, ambao wamekubaliana nasi, kwamba hawa watu kwa kifupi wanatambulika na wapatiwe malipo yao kwa kadhia waliyopata,” alisema Amelie Oudea-Castera kwenye kikao na waandishi wa habari.

Alisema kulikuwa na tiketi 2700 ambazo hazikuwa zimepitishwa kwa ajiri ya kuingia uwanjani, ambazo bado zilikuwa kwenye mfumo na walinyimwa kuingia uwanjani.


SHINDA SAMSUNG A32 NA AVIATOR

SHINDA Samsung A32 ukiwa na mchezo wa Aviator kwenye Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet! Kwea pipa ukusanye zawadi zako pamoja na ushindi mnono wa mkwanja!

kasa wa njano, Kasa wa Njano Awapa Ubingwa wa CL Liverpool., Meridianbet

SOMA ZAIDI HAPA

Acha ujumbe