FAI Kutoa Tiketi 2000 kwa Wakimbizi wa Ukraine

Chama cha soka nchini Ireland FAI kimepanga kutoa tiketi 2000 kwa wakimbi wanaotoka nchini Ukraine ambao wanahifadhiwa nchini humo kwa ajiri ya kuangalia mchezo kati ya Ireland dhidi ya Ukraine.

FA Irish pia imepanga kuchangia kiasi cha  €100,000 kwa chama cha msalaba mwekundu cha nchini, ambacho kimewakalimu wakimbizi hao kutoka nchini Ukraine, ambapo pesa hizo zitatokana na mauzo ya tiketi ya kwenye mchezo huo.

FA Irish watatoa tiketi hizo kwa wakimbizi waliofika hivi karibuni ambao wanaishi nchini humo kutokana na matatizo ya vita iliyosababishwa na taifa la Urusi kuivamia nchi hiyo.

FAI walisema watawasiliana moja kwa moja na kundi la wakimbizi hao na hususani grassroots football clubs, ambao wamewakaribisha wakimbizi hao hivi karibuni kwenye janii yao.

“Kwa niaba ya bodi na wafanyakazi wa FAI na kila mmoja anayehusika kwenye mchezo wa mpira wa miguu nchi Ireland, nina furaha ya kutangaza kwamba, tunawaalika wakimbizi 2000 wa Ukraine ambao tayari wako Ireland, kuja kwenye mchezo na kutaza timu yao kwenye uwanja wa Aviva mwezi ujao.

“Pia ningependa kuthibitisha kuchangia kiasi cha  €100,000 kwa chama cha msalaba mwekundu kusaidia kuwakarimu wayukraine, na pesa hizo zitatoka kwenye mauzo ya tiketi ya mchezo huo,” mkurugenzi wa FIA Jonathan Hill alisema.


TENGENEZA FAIDA NA ZEUS ANCIENT FORTUNES

Una Kila sababu ya kufurahia wiki yako na kutengeneza mwaka huu uwe wa faida zaidi katika kasino zetu za mtandaoni za meridianbettz. Mchezo wa Zeus Ancient Fortunes unakuongoza kutekeleza hilo.

tetesi, Tetesi za Soka Barani Ulaya., Meridianbet

CHEZA HAPA

Acha ujumbe