Mchezaji wa kimataifa wa Tanzania Simon Msuva anayekipiga katika klabu ya Al Qadisiya inayoshiriki ligi daraja la kwanza ya Saudi Arabia amefungua mlango wa magoli baada ya kufunga goli kwenye mechi ya kwanza ya msimu mpya wa ligi hiyo.

Msuva aliipatia timu yake goli la kusawazisha mnamo dakika ya 60 na kufanya ubao wa matokeo kusomeka 2-1 ambao mechi iliisha kwa timu yake kupoteza kwa 3-1 dhidi ya Al Akhdoud ambao wapo kileleni mwa msimamo wa ligi daraja la kwanza ya Saudi Arabia.

View this post on Instagram
Msuva amesajiliwa na timu hiyo baada ya kushinda kesi yake na waajiri wake wa zamani ambao ni mabingwa wa ligi ya mabingwa barani Afrika CAFCL ambao walifikishana kwenye mahakama ya FIFA kudai malipo yake ya mshahara na posho zingine.
katika kikosi hicho yumo pia aliyekuwa mshambuliaji wa Al Ahly ya Misri Walter Bwalya ambaye nae alitemwa na miamba hiyo ya Misri.


