Arteta na Lampard: Kesho Inayong'ara

Vijana wa Mikel ArtetaArsenal watakutana na kikosi cha Chelsea kinachonolewa na Frank Lampard katika fainali ya Kombe la FA Agosti 1, 2020.

Mchezo huo utawakutanisha makocha wawili wadogo kwenye Ligi Kuu UingerezaArteta (38) na Lampard (42). Mchezo huu utakuwa wa aina yake kutokana na uzoefu wa makocha hawa ambao kila mmoja ameshawahi kubeba Kombe la FA wakati walipokuwa wachezaji.

Lampard amebeba Kombe la FA mara 4 alipokuwa mchezaji wa Chelsea, wakati Arteta akilibeba kombe hilo mara 2 alipokuwa anaitumikia klabu ya Arsenal.

Arteta na Lampard wamekuwa na msimu mzuri kwenye Ligi Kuu – EPL wakijitahidi kuvinoa vikosi vyao. Uwezo wao wakuongoza vijana na kuwasimamia mchezaji mmoja mmoja lakini pia mbinu za matumaini na morali, zimewasaidia kwa kiasi kikubwa katika kazi zao kwa msimu huu.

Frank Lampard ambaye amekuwa akitumia mfumo wa 3-4-3 kwa kiasi kikubwa, ameweza kuingoza Chelsea mpaka kumaliza katika nafasi ya nne kwenye msimamo wa Ligi Kuu Uingereza- EPL na kufuzu hatua ya fainali ya Kombe la FA.

Japokuwa anaonekana ni kocha mtaratibu, Lampard amefanikiwa kutumia uwezo wake wa kuongoza wachezaji mmojammoja ndani na nje ya uwanja. Jambo hili limemsaidia katika kufanya maamuzi ambayo kwa namna moja ama nyingine yalimpatia matokeo katika michezo mbalimbali.

Mchezaji kama Olivier Giroud alionekana kama hana nafasi tena katika kikosi cha Chelsea na wengi kutazamia kuondoka kwa mshambuliaji huyo. Lampard amefanikiwa kwa kiasi kikubwa kurudisha morali na ari ya uchezaji wa Giroud na sasa tunamuona Giroud ambaye amekuwa akiongoza mashambulizi ya Chelsea na kuisaidia timu kupata matokeo.

Arteta nae amejitahidi kwa upande wake hasa tukiangazia suala zima la mchezaji Mesut Ozil ambaye amekuwa na wakati mgumu kwenye kikosi cha Arsenal kwa muda sasa. Arteta aliamua kumuacha Ozil katika mechi kadhaa, lengo likiwa ni kumpatia changamoto zaidi mchezaji huyo ambaye ni dhahiri ameshuka kiwango.

David Luiz ambaye ameonekana kushuka kiwango na kusababisha timu kukosa matokeo katika mechi muhimu kama ya Manchester City (3-0). Arteta amekuwa akimkingia kifua mchezaji huyo na kumuamini, Luiz alionesha uwezowake na kuisaidia timu yake kufuzu fainali ya Kombe la FA alipokutana na Manchester City katika nusu fainali na kushinda kwa magoli 2-0.

Arsenal na Chelsea watakutana tena katika dimba la Wembley mapema Agosti 1, 2020 watakapokuwa wakiwania Kombe la FA ambalo ni kombe muhimu kwa makocha hawa na timu wanazoziongoza. Kwa Arsenal, kubeba kombe hili itakuwa ni tiketi ya kushiriki michuano ya Europa msimu ujao na hivyo kuufanya mchezo huu kuwa na umuhimu wa aina yake.


Nini kinachokupa raha kama michezo ya kasino ya mtandaoni? Hasa unapojua kuwa kuna ushindi, jackpot na mizunguko kibao ya bure. Ungana na bwana Meridian kupata ushindi na burudani.

Cheza Hapa Sasa

44 Komentara

    Asante kwa makala nzuri#Meridianbettz

    Jibu

    Utakuwa usiku muhimu sana kwa wote wawili kuimarisha imani ya bodi na mashabiki kwao. Ni vigumu kutabiri nani mshindi mpaka dakika 90 zitakapotamatika#meridianbettz

    Jibu

    Arsenal wamekuwa na msimu mbaya lakini cha ajabu wanaweza wakaibuka bingwa katika FA

    Jibu

    Hii mechi sio ya kutabili mchawi dakika 90 maana inaonekana ngumu sana kila mmoja analitaka kombe la FA

    Jibu

    Asante kwa makala nzuri

    Jibu

    Mtanange ninao usubuiria kwa hamu zote

    Jibu

    Mtanange huu usinipite navyo usubilia kwahamu utanipa pesa huu

    Jibu

    Huo mtanang’e nausubili kwa hamu#meridianbettz

    Jibu

    Luiz amekua na makosa mengi kipingi hiki ila arsenal wangempa mda tu

    Jibu

    Tunasubiri Kwa hamu

    Jibu

    Tunasubiri

    Jibu

    Makala ipo powa

    Jibu

    Vigumu kutabiri mshibdi mpira dakika 90

    Jibu

    Arteta hii mechi atashinda sababu Arsenal Wana history nzuri Sana katika hiki kombe la FA ushindi kwake ni lazimaa

    Jibu

    Ni mechi ya kukatana shoka hatumwii mtoto dukani.

    Jibu

    Tunasubili kwa hamu hii sio ya kukosa

    Jibu

    Nimechi kabambe

    Jibu

    Kazi kwao sisi macho uwanjani tukishuhudia mtanange huu mkali

    Jibu

    Good newz

    Jibu

    Hii kali sana

    Jibu

    Gud news 👍

    Jibu

    Hii mechi sio ya kukosa.

    Jibu

    Tutashuhudia fainali ngum na ya kuvutia hapa

    Jibu

    Hii mechi naitakia ushindi timu ya lampard naamini itafanya vema

    Jibu

    Imeeleweka hii

    Jibu

    Hapa n pata shika nguo kuchanika atumw mtt dukan

    Jibu

    Ni vigumu kutabir mechi iyo

    Jibu

    asante meridianbet kwa habar moto moto

    Jibu

    Mechi kalii Sana ngoja tujionee wenyewe

    Jibu

    Arsenal wakaze watufurahishe mashabiki

    Jibu

    Kazi ipo!

    Jibu

    Hii mechi ni Kali Sana tunasubili kwa hamu

    Jibu

    Unasubirika kwa hamu japo mwamuz dkk 90

    Jibu

    Arteta hii mechi atashinda sababu Arsenal Wana history nzuri Sana katika hiki kombe la FA ushindi kwake ni lazimaa

    Jibu

    Chelsea anashinda hii mechi

    Jibu

    Hii itakua bonge la mecha sana kama wanakutana José morihno na asene wenger

    Jibu

    Maoni:Patachimbika

    Jibu

    Gud news

    Jibu

    hapa leo nyasi lazima ziote moto

    Jibu

    Nyasi zitawaka

    Jibu

    Wacha tuonee

    Jibu

    Utakuwa usiku muhimu sana kwa wote wawili kuimarisha imani ya bodi na mashabiki kwao

    Jibu

    Kweli kabisa hawa jamaa watangara sana badae

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.