Robert Lewandowski anaamini anaweza kuendelea kusakata kabumbu mpaka pale atakapo fikisha umri wa miaka 40 baada ya kuendelea kuwa sehemu ya kikosi cha Bayern Munich kwa msimu mwingine.
Mshambuliaji huyo wa Bayern Munich alifunga magoli 55 msimu uliyopita 2019-20 na kuisaidia timu ya Bayern kushinda mataji matatu ndani ya msimu mmoja, na kufanikiwa kutwaa taji la Champions League kwa mara ya kwanza katika maisha yake.
Lewandowski hajaonesha dalili yoyote na kustaafu na wiki illiyopita alisema mkataba wake na Bayern Munich unaofika tamati mwaka 2023 “Haitakuwa ndiyo mwisho”.
Akiwa na umri wa miaka 32, Lewandowski aliiambia Kicker ataendelea kucheza huenda ikawa miaka nane ijayo.

Alisema: “Kumaliza soka langu ndani Bayern Munich ndiyo chaguo, bado nina muda wa miaka mingi kucheza”.
“Sifikirii kuhusu kustaafu kwa sasa.
“Sijihisi kama nina 32 najihisi poa kama wakati nikiwa na miaka 26, nilifanyia kazi kile nilichokuwa natamani nikipate miaka ya hivi karibuni.
Licha ya kuwa na msimu bora, Lewandowski hakufanikiwa kuwa mfungaji bora wa ulaya na kushinda kiatu cha Dhahabu baada ya kupitwa upachikaji magoli na Ciro Immobile wa Lazio aliyefunga magoli 37 wakati Lewandowski akitikisa nyavu mara 34 Bundesliga.
“Nafikiri ni aibu Bundesliga kuwa na michezo michache kuliko Serie A [ Bundesliga ina michezo 34 wakati Serie A ipo michezo 38],” alisema Lewandowski.
SHINDA NA HI LO
Sasa hii ni rahisi zaidi kupata USHINDI! Unatabiri karata ipi ipo chini au juu, kisha unakusanya mkwanja wako.


Furahav
Huo ni uamuzi mzuri sana.
Hidaya
Kikubwa uhai
Issa
Lewandoski bado yupo poa kwa spidi alionayo hilo ni rahisi
magdalena
maamuzi yake yapo sahihi umri ni mkubwa sana
Mwanahamisi
Huo ni uamuzi mzuri sana
aisha
Safi sana broo nakukubali sana maana unajielewa
Amiri Kayera
Kwa umli wake cjui km atafik huo umli
Samiah
Kikubwa dua
rama
safii endelea kutupa burudani mashabiki wa mpira
Hope mwaikuka
Ni vzur tu maana uwezo ni wako
Adelta
Ni vizuri sana 👍@meridianbettz
Sadick
Thiago Silva nae amesema anataka kufikia record ya Paulo Maldini kwa kucheza mpaka miaka 40. Anachotakiwa Lewandowsk ni kujitunza na kuepuka majeraha#meridianbettz
Mwajumah
Huo ni uwamuzi mzuri sana#Meridianbettz
felister
yupo sahihi maamuzi mazuri
Lydia Emmanuel Magoti
Nivizuri Sana kwalicho kiongea Lewandowski kwasababu mwili wake bado unadai kupiga kazi
Sabrina
Sio mbaya amejiwekwea muda wa kustaafu atakua kashafikia malengo yake
Ernest
Lewandowski bado yupo vizuri huenda akaendelea kukipiga adi kufikia umri huo
Theonestina
Kama bado uko fit haina shida
Antony Luseno
Kila jambo ni malengo
Khadija
kila la kheri kwake
Tatu
Muda ukifika ukifika auna jinsi itabidi uwapishe wezio
Rehema
Kila la kheri
Fatina mfigi
Maisha popote
lombo
mambo ni moto na meridianbet
Rose kapinga
Kazi na umrii!!!
Rehema Dickson
Allah awe nae dua nyingi sana kwake
marry
kila la kher
Agness
Nimaamuzi mazuri
Janeflora malisa
Kila la kher
farida ahmadi
Maamuzi mazuri Sana
Samira
Ajitunze na kuepuka majeraha zaidi itamsaidia kufikia lengo la miaka 40
Shafii
Kwa uwezo aliokua nao anaweza akafika hiyo miaka.
Theckla
Yote yanawezekana
Ester jackson
Duuh sasa anataka kucheza na Mpira magoti huyu
Saupha mohamed
Uwamuzi mzuri
Dorophina
Hapo yy na nguvu zake alizonazo anaweza akafika umri huo
Caroline
Kikubwa nidhamu ili usipate majeraha
Zeiyana
Lewandowski hana mchango mkubwa pale Bayern munch ukiangalia mri wake humeenda lakini hanauwezo mkubwa sana
David Pere
Thiago Silva nae amesema anataka kufikia record ya Paulo Maldini kwa kucheza mpaka miaka 40. Anachotakiwa Lewandowsk ni kujitunza na kuepuka majeraha
Salma ngende
Maamuzi mazuri
Povel
Maamuzi yake
Neema
Kama bado yuko fitiii azidii kucheza tu
Faraja molell
Ni maamuzi mazur kujituma ndo la muhim
Nasra
Kwa kiwango chake alicho kionesha 2019-2020 anaweza akafika huko.
Shani
Lewandoski fowad makin San kaki washa msimu huu
Latifa juma mohamed
Kazi na umri, vzr
Genia Sikaluzwe
Ni Jambo jema hilo
Gabriel
Yuko sahihi kabisa
Tahiya
Mpira bhana una mambo mengi kuna kuumia ukashindwa kutimiza ndoto zako ila kikubwa ni kumuomba Mungu
warda
Yupo fit sana