Werner Akerwa na Matokeo ya Sare Dhidi ya Spain.

Mshambuliaji wa Ujerumani Timo Werner ameudhika kufuatia timu yake kuruhusu goli la dakika za majeruhi na kufanya mchezo kumalizika kwa 1-1 dhidi ya Spain katika michuano ya Nations League.

Werner alifunga goli la kuongoza dakika ya 51 ya mchezo Ujerumani wakiwa wanatafuta ushindi jijini Sturttgart siku ya Alahamisi, lakini Jose Gaya wa Hispania aliisawazishia timu yake dakika ya 95.

Nyota huyo wa Chelsea Timo Werner, ambaye anajiandaa kwaajili ya msimu wake wa kwanza akiwa Stamford Bridge baada ya kutua akitokea RB Leipzig, ameonesha kutolizishwa na matokeo kwani Ujerumani ilikuwa ikihitaji ushindi katika mchezo huo.

“Ni maudhi kwa sababu tumecheza kwa bidii kubwa sana,” Werner alisema baada ya mchezo kuisha.

“Baada ya goli tuliruhusu sisi wenyewe kurudi kucheza nyuma na kufanya wapinzani wapate nafasi kadhaa upande wetu.”

Kwa Matokeo hayo yanaacha Ujerumani iendelee kutafuta ushindi wao wa kwanza katika michuano hiyo baada ya kutoa sare mbili na kupoteza mchezo mmoja mwaka 2018-19.

Kocha mkuu wa Ujerumani Joachim Low aliongeza: “Nimeridhika na nilichokiona, vijana wetu wametuonesha walichokua nacho mpaka mwisho.

“Kwa upande wangu ni muhimu kutowaruhusu Spain kucheza na maoni yangu tulikuwa na nafasi nyingi, lakini kipindi cha pili hali ilikuwa ngumu kidogo.

Nyota wa Atalanta Robin Gosens pia alicheza mchezo wake wa kwanza akiwa na timu ya taifa ya Ujerumani na ndiyo aliyetengeneza asisti ya goli la Werner aliiambia UEFA.com “Ulikuwa ni usiku maalumu, mchezo wangu wa kwanza kucheza kama beki tatu, nafasi ninyocheza nikiwa Atalanta kwa hiyo ilikuwa rahisi kuimudu.


SHINDA NA HI LO

Sasa hii ni rahisi zaidi kupata USHINDI! Unatabiri karata ipi ipo chini au juu, kisha unakusanya mkwanja wako.

Cheza sasa

36 Komentara

    spain wameniudhi sana jana wamejua kunichania mkeka wangu

    Jibu

    Hii inaonyesha kuwa wachezaji wa Chelsea msimu huu hawataki kabisa mchezo sio Werner tu hata sisi mashabiki kutokana na usajili tulio nao tunataka ushindi zaidi lakini kama Chelsea wakiongeza mabeki na kumleta kipa mwingine tutakuwa tumekamilika kila idara ila hasaivi bado ingawa tunawachezaji wazuri

    Jibu

    Kocha wa Joakim Low anatakiwa kujitazama,hana jipya,Ujerumani inashuka viwango badala ya kupanda#meridianbettz

    Jibu

    Chelsea wakiongeza mabeki na kumreta kipa mwengine tutakuwa tumekamilika kila idara ingawa sasahiv tunawachezaji wazur

    Jibu

    huo ndo mpira inabidi akubaliane na matokeo tu haina jinsi sio yeye peke yake aliyekerekwa lakini hatuna budi

    Jibu

    Wachezaji wa chelsea inaonyesha hawataki kabisa mchezo sio werner tu ata ss mashabiki#Meridianbettz

    Jibu

    Ndo matokeo hayo unabudi kukubariana nayo!

    Jibu

    Matokeo hayalizishi

    Jibu

    Huu sio muda wa kulaumiana yaliyotokea yametokea.waangalie walipokosea wajirekebishe

    Jibu

    Wakaze buti, matokeo hayaridhishi

    Jibu

    Kijana bado hajajifunza tuu kuwa mpira ni dakika 90?

    Jibu

    Timo Werner naona ajakubaliana na matokeo ya timu yake ya kutoka sale hii inaonyesha jinsi gani anamapenzi ya dhati na timu yake

    Jibu

    Mashabiki hatujafurahi matokeo
    @meridianbettz

    Jibu

    Hayo ndio matokeo inabidi wakubaliane na hali asiye kubali kushindwa sio mshindani

    Jibu

    Hayo ndio matokeo lazima wakubaliena nahali halisi kila mtu kapambana kwajudi zao zote nampila kila mtu kaupika kwaio kila mtu lango lake lilikaza kwahio kilamtu akubali Kama alishindwa kuliona lango lamwenzie kupataushindi wamoja kwamoja

    Jibu

    ndo moja wapo ya matokeo ya mpira

    Jibu

    Inapaswa aelewe kwamba mpila unamatokeo matatu ushindi,kupoteza na sare kwaiyo wajipange kwa mechi ijayo.

    Jibu

    Hakuna namna hapo ni kkubali matokeo tu

    Jibu

    Ni lazma wa kubaliane na matoke

    Jibu

    Ndo mpira ulivyo.

    Jibu

    Germany ya kipind hiki ni moto sana

    Jibu

    Juhudi za ziada zinaitajika na mazoezi ya kutosha kama wanataka kubadili matokeo!!!

    Jibu

    Mpira huko na matokeo matatu kubali tu

    Jibu

    Mpira kazima uwe na matokeo ya kushinda au kushindwa so akubali matokeo

    Jibu

    Werner game ya jana uzoef wa Spain uliwafany wapate goli dakika ya mwisho

    Jibu

    Mpira dakika 90 hiyo ni kawaida kikubwa kujiweka sawa katika kikosi

    Jibu

    Ndio mchezo ulivyo akubaliane na matokeoo

    Jibu

    Mpira unamatokeo matatu kufunga,kufungwa na kusuruhu na asiekubali kushindwa sio mshindani

    Jibu

    Mpr dk 90 na una matokeo matatu kufungwa kushinda sare co kama utakubaliana na matokeo yyte utakuwah co mshindani

    Jibu

    Ndo matokea ya mpila kila Mt anatak ushind

    Jibu

    Bahati haikua yakwao japo walicheza vizuri sana

    Jibu

    Chelsea msimu huu hawataki kabisa mchezo sio Werner tu hata sisi mashabiki kutokana na usajili tulio nao tunataka ushindi zaidi lakini kama Chelsea wakiongeza mabeki na kumleta kipa mwingine tutakuwa tumekamilika kila idara ila hasaivi bado ingawa tunawachezaji wazuri

    Jibu

    Mambo ya sare Mie siyapendagi

    Jibu

    Ni matokeo ilimpasa akubaliane nayo

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.