Kunako msimu wa NBA, michezo ya Eastern na Western Conference imemalizika na sasa washindi – LA Lakers na Miami Heats kuanza kuchuana ili kumpata mbabe wa NBA 2020.
Katika mchezo wa Eastern Conference, Miami Heats walikuwa wakichuana na Boston Celtics. Mchezo ambao ulikuwa na jumla ya michezo 7 na umehitimishwa kwa michezo 6 baada ya Miami Heats kuibuka kidedea kwa matokeo ya 4-2 katika michezo hiyo.
Miami Heats ambao ni washindi wa NBA mara 3, sasa wanatinga hatua ya fainali kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2014. Mchezo wao uliomalizika kwa ushindi wa pointi 125-113 umepeleka kilio kwa Boston Celtics ambao wanapoteza fainali ya 3 mfululizo.

Bam Adebayo alikuwa shujaa wa Heats kwa kupachika pointi 32 na kucheza mipira 14 iliyokufa. Adebayo amejisafisha kibabe kwa kile alichokifanya katika mchezo wa 5 ambapo aliwagharimu wachezaji wenzake.
“nilipaswa kujipanga kivingine na kuonesha kile ninachohitaji kuwa na nimefanya hivyo usiku wa leo. Kuwepo katika hali ile na kujifunza kutoka pale, kuisaidia timu kushinda fainali na kusonga mbele, ni kitu kikubwa kwangu.” amesema Adebayo.
Kwa upande wa LA Lakers, LeBron James ameisaidia timu yake kufika fainali ya NBA baada ya miaka 10 kwa ushindi wa pointi 117-107 dhidi ya Denver Nuggets.
Ushindi wa jana, umewapatia matokeo ya jumla ya 4-1 katika michezo 5 na sasa wametinga hatua ya Fainali ya NBA 2020.
LeBron James alikuwa shujaa wa Lakers kwa kupachika pointi 38 na kucheza mipira 16 iliyokufa huku akitoa pasi 10 za magoli.

LaBron James anakuwa ni mchezaji wa 4 wa kucheza fainali 10 za NBA na hii ni mara yake ya kwanza akiwa na Lakers.
“Ninafuraha kubwa kuwa sehemu ya timu hii na kuisaidia kurudi katika nafasi yake,ambayo ni kucheza kwenye fainali.” amesema LeBron James.
Mchezo wa kwanza wa fainali utachezwa Jumatano.
Beti kwa Kitochi Kushinda 300,000,000!
Unajua kuwa unaweza kushinda milioni mia tatu kwa buku tu? Ndiyo! Unaweza kushinda kwa kupiga *149*10# na kubashiri. Ingia mchezoni!


Povel
NBA mambo ni moto. VITA ya james le Bron vs Bam Adebayo🔥🔥🔥🔥🔥🔥
magdalena
lakers wapo vizuri sana wakiitumia vizuri nafasi yao wanaweza kuibuka na ubingwa
Adelta
Wapo vizuri
Fatina mfigi
Safii
Ernest
Namuona LeBron kama MVP ndani ya NBA
Mwajumah
NBA kumenoga
Tatu
Laker wapo vizuri ili pambano litakuwa la nguvu
Zeiyana
Mchezo utakua mgumu sana kwa Lakers maana heats wapo vizuri sana wanamolali ya kuchukua ubingwa toka 2014 hii nafasi himekua kama bahati kwao sijui kama wataipoteza
Angelina
NBA sio mchezo lakers hawamwachi mtu salama
Lydia Emmanuel Magoti
NBA kumepamba moto patakuwa apatoshi
Hidaya
NBA kumekucha
aisha
Lakers naona kama ndio watakao pata ubingwa
Salma ngende
Wapo vizuri
Dorophina
NBA Mambo mazuri
Mariam mtandama
Wapo vizur
Khadija
NBA kumenoga
Elika
Naiaminia sana Lakers maana kiwango chai kipo juuu
Neema
Mambo yanazidii kunoga
Janeflora malisa
Asnt kwa taarif
Shani
LeBron na Davis wanaweza kuuzuia moto wa hearts
Mwanahamisi
Wapo vizuri
Hopemwaikuka
Wacha ww
Gabriel
NBA Mambo mazuri
Fatuma kasomo
Gud news
lombo
mambo ni moto na meridianbet
Samira
NBA imepamba moto kwakweli
Amiri Kayera
Utakua mpambano mkali
Theonestina
Safiii
Theckla
Kila la kheri kwao
Issa
Lakers ni noma sana
Sabrina
Lakes jeshii
Saupha mohamed
Lakes nomaa
Samiah
Kila lakheri kwao
Nasra
Kumenoga NBA
Rose kapinga
Hatariiii
felister
wapo vizuri
Latifa juma mohamed
NBA kumekucha
David Pere
NBA mambo ni moto. VITA ya james le Bron vs Bam Adebayo