Promota wa Tyson Fury, Bob Arum, amefichua kuwa Anthony Joshua atachapana na Oleksandr Usyk mwezi Juni mwaka huu.
Mazungumzo kuhusu bingwa wa taji ambaye hajawahi kupingwa kati ya Usyk na Fury yalibuma hivi majuzi, na kusababisha Joshua na Usyk kusonga mbele na pambano lao la marudiano.
Ingawa pambano lilikuwa limedokezwa Aprili, Arum alirekebisha madai hayo.
“Watapigana mwezi Juni,” aliiambia FightHype kuhusu Joshua na Usyk.
Pambano lao la kwanza lilifanyika kwenye Uwanja wa Tottenham Hotspur ambapo bondia huyo wa Ukraine alimdunda Joshua kwa point.
Dakika tano pekee zinakutosha kuwa mmoja wa washindi wa mkwanja mrefu ndani ya kasino pendwa ya meridianbettz katika sloti maridhawa ya KENO, moja ya michezo inayoipa thamani dau lako.


