Baada ya kupoteza michezo miwili kunako nusu fainali ya NBA, Western Conference. LA Clippers wamerejea mchezoni kwenye mchezo wa tatu wakiwa nyumbani.
Kabla ya mchezo wa 3 dhidi ya Utah Jazz, Clippers walikua wameshapoteza michezo miwili ya awali kati ya 7 watakayocheza. Hakika huu ulikua ni mchezo ambao Clippers waliingia wakiwa na kila uhitaji wa ushindi.
Ubora wa Kawhi Leonard na Paul George, ulihitajika katika kufanikisha lengo la Clippers kujiwekea matumaini ya kufuzu hatua ya fainali ya NBA kwa upande wa Western Conference.

Matokeo ya pointi 132-106 yaliwatosha Clippers kupata ushindi wa kwanza kati ya michezo mitatu. Leonard na George walipachika jumla ya pointi 65 na kupeleka furaha kwa kocha wa Clippers, Tyronn Lue.
” Ninahitaji wachezaji wangu bora wawili ili kuweza kufanya hivyo (kushinda). Wanaweka mfano kwa kila mmoja.” alisema Lue baada ya ushindi dhidi ya Jazz.
Mchezo wa 4 utachezwa Jumatatu usiku.
Chukua namba yako ya akaunti na kiasi cha pesa unachotaka kuweka, sogea kwenye duka lolote la Meridianbet lililo karibu nawe utasaidiwa kuweka pesa.


