Legendari wa ndondi, Conor McGregor amebainisha kuwa mpango wake ni kuhakikisha anaongeza utajiri wake ili aweze kuungana na mastaa kama Ronaldo, Messi na Mayweather ambao ni mabilionea.
Katika mpango wake huu, bondia huyu ambaye anatarajiwa kurejea ulingoni hivi karibuni, amejiwekea malengo ya umri ambao ni lazima awe amefikia ubilionea.

Bingwa huyu kwa sasa ana miaka 32, na amejipatia miaka 3 tu kuufikia ubilionea. Nyota huyu kwa sasa anatajwa kuwa na utajiri wa takribani Euro milioni 100. Anahitaji kuwa Bilionea hadi anapofikia miaka 35, umri ambao mastaa wengi wa michezo hustaafu.
McGregor ambaye ni bondia anayelipwa pesa nyingi zaidi katika historia ya UFC Lightweight, anatarajia kurejea ulingoni mapema 2021.
Ukiacha kuwa moja ya wapiganaji wanalipwa pesa nyingi zaidi, Staa huyu pia ana madili na kampuni mbali mbali za kibiashara kama Burger King, Beats by Dre, Monster Energy na Reebok. Anaamini anaweza kuongeza thamani na kupata malipo bora zaidi yatakayofanikisha lengo lake afikiapo umri wa miaka 35.
Hii ni halisi kwa ajili ya mashujaa wote! Ukiwa jasiri unavuna mkwanja kibao hapa na sloti hii ya Huangdi Casino. Waka nusu tukupe maradufu!



Povel
Inawezekana kikubw juhudi,bidiii, maarifa,mshikamano ,na kutok kutaka tamaa na kuwa na imani na jambo fulan hunawez kufik malengo uliojiwekeah hapo
Shani
Inawezekana juu ana nia sasa awekeze nguvu zake kwny mapambon!!
Fatina mfigi
Ukikaza buti mbona utafikia malengo yako Mcgregor na kuwapit mbak hao!
Sauda
Kila la kheri kwake.
warda
Kila unaloomba ndo Mwenyezi Mungu anavyokupa
Sadick
Kupanga malengo ni jambo zuri na kufanikisha malengo ni jambo jingine. Kila lakheri kwake kufanikiwa lengo lake
aisha
Mc gregory makin sana kwenye ngumi
Hopemwaikuka
Pambana tu utafika hakuna shida
Issa
Gregory anawez kua tajir sana kwa mapambano alioyaweza
Saupha mohamed
Mawazo mazurii sana apambane tu
Ester jackson
Kila nia kuna ufahari mbeleni ila duuh ametisha yani sisi binadamu huwezi kuwa maarafiki ambao wako juu zaidi yako kama huna chochote hayo ndio matabaka ambayo tuliyo wekewa tajiri na tajiri mwezake masikini na masikini mwezake .
Elika
Hayo ndio maendeleo
Adelta
Wazo zuri apambane ili ndoto yake itimiye
Mwajumah
Kila la kheri kwake kikubwa apambane tu
Caroline
Kila kitu kinawezekana chini ya jua..apambane tyu
Tatu
Kuwa na malengo ni jambo zuri
Angelina
Penye nia pana njia
Fatuma kasomo
Kila la kheri
Sabrina
Namtakia heri na mafanikio
Sabrina
Ndoto zake zitatimia tu
Zahara Omary
Kula la kheli
Tahiya
Good news
magdalena
kikubwa ni kutimiza ndoto zake