Baada ya kutawazwa rasmi kuwa Mabingwa wa AFCON 2025, Morocco Simba wa Atlas wameamua kusherehekea kwa staili ya kipekee. timu ya taifa imezindua jezi maalum za ubingwa, zinazotambulisha mafanikio yao ya kihistoria ya ubingwa wa ‘mezani’.
Jezi hii mpya inajivunia nyota ya pili kifuani, ikiwakilisha ushindi wao wa pili wa AFCON baada ya miaka mingi ya kusubiri. Kwa mara ya kwanza, nyota hii inakiri historia na mafanikio mapya ya timu ya taifa.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Ubunifu wa kitamaduni umejumuishwa kwenye jezi kwa kutumia nakshi za ‘Zellij’ sanaa ya vigae vya kimoroko vilivyochorwa kwa ustadi kwenye mabega na upande wa ubavu, ikionyesha utambulisho wa taifa na urithi wa kiutamaduni.
Aidha, nembo ya CAF pamoja na namba za wachezaji zimepambwa kwa rangi ya dhahabu inayong’ara, ikionyesha utukufu wa ubingwa huu na kuimarisha heshima ya Morocco barani Afrika.
Jezi hizi za kipekee sasa zinatumika kusherehekea ushindi wa Morocco, huku zikionyesha fahari, historia, na utamaduni wa taifa lililoongoza kwenye soka la Afrika.

