Mchezaji wa kimataifa wa Argentina Lionel Messi amesema kwamba baada ya michuano ya kombe la Dunia kumaliza atafanya uchaguzi upya kama ataendelea na timu ya taifa au atastaafu.
Mshambuliaji huyo wa Paris Saint-Germain mwenye umri wa miaka 35 alihusika katika ushindi wa Argentina wa 3-0 dhidi ya Venezuela usiku wa kuamkia Jumamosi mchezo wa kufuzu kombe la Dunia 2022 Qatar.
“Baada ya kumaliza kwa kombe la Dunia nitatafakari upya mambo mengi itategemeana kama tutamaliza vizuri au vibaya, acha tutumaini yataenda vyema.
“Kuna kundi kubwa la watu hapa na kila siku wanazidi kunionyesha mambo makubwa zaidi. Nashukuru sana, haiwezi kuwa mimi tu kila wakati nikija Argentina.
Staa huyo wa Argentina alifanikiwa kutwaa taji la kwanza la kimataifa na timu ya wakubwa Copa America msimu mwaka 2021 na kwa sasa amelenga kutwaa kombe la Dunia 2022.
3500 NI YAKO UKIJIUNGA TU MERIDIANBET!
Una nafasi ya kupata bonasi ya shilingi 3500 kwa ajili ya kuanza safari yako ya kasino ya mtandaoni ya Meridianbet.