Shirikisho la mpira wa miguu duniani FIFA huenda likabadilisha tarehe ya kuanza michuano hiyo baada ya taifa mwenyeji kuomba kubadilishwa kwa tarehe ya kuanza kwa michuano hiyo miezi mitatu kabla ya michuano hiyo kuanza.
Mashindano ya kombe la dunia kwa mara yanafanyika ukanda wa arabia kwenye kipindi cha baridi badala ya majira ya kiangazi kama ilivyozoeleka. Tarehe ya awali iliyopangwa kuanza kwa mashindano hayo ni 21 septemba na mchezo wa kwanza ni Senegal dhidi ya Uholanzi jijini Doha.

Qatar wamepeleka mapendekezo ya kufanya mabadiliko ya ya mashindano hayo, ambapo mwenyeji ameomba tarehe irudishe nyuma mkwa siku moja ili waweze mwenyeji aweze kucheza tarehe 20 novemba kwenye mchezo wa ufunguzi.
Ili maombi ya Qatar yaweze kukubaliwa FIFA wanapaswa kukaa kikao na mashirikisho ya mpira ya mabara yote yaweze kuidhinisha mabadiliko hayo kabla ya kupitisha mabadiliko hayo rasmi.

