Frenkie de Jong: Manchester United Waweka Mezani Ofa Yao

Klabu ya Manchester United imeripotiwa kuwasilisha ofa yao ya kwanza kwa kiungo wa Barcelona Frenkie de Jong. 

Mholanzi huyo amekuwa katikati ya vichwa vya habari akihusishwa na kuhamia Old Trafford msimu huu wa joto, licha ya viashiria kuwa anataka kusalia Barcelona.

Ripoti ya awali ilionyesha kuwa Mashetani Wekundu walikuwa bado hawajawasilisha ofa rasmi kwa mchezaji huyo wa zamani wa Ajax.

Hata hivyo, kwa mujibu wa Marca, Manchester United wamewasilisha ombi lao la awali kufungua biashara hiyo, ambalo linasemekana kuwa na thamani ya €60m (£51.3m) pamoja na nyongeza ya €20m (£17.1m).

Licha ya kuwa hakuna dili lililokubaliwa, ofa hiyo imeripotiwa kupokelewa vyema na Barcelona, ​​ambao wanataka kupunguza mzigo wa mishahara ili waweze kusajili wachezaji wapya msimu huu wa joto.

Huku De Jong akiripotiwa kulipwa €40m (£34.2m) katika muda uliosalia wa kandarasi yake Barcelona, ​​kumtoa mchezaji huyo wa kimataifa wa Uholanzi kungesaidia wababe hao wa Catalan kuboresha hali yao ya kiuchumi.

Frenkie de Jong: Manchester United Waweka Mezani Ofa Yao
Frenkie de Jong

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25, ambaye anaweza kuungana tena na kocha wa zamani wa Ajax Erik ten Hag, amefunga mabao 13 katika mechi 139 alizochezea Barcelona.


ALIYA’S WISHES

Bila shaka unatamani ushindi mkubwa, vipi kuhusu kujaribu Sloti hii ya Aliya’s Wishes? jaribu ushinde sasa. Kasino ya Mtandaoni

CHEZA SASA

Acha ujumbe