Klabu ya Chelsea imeonyesha nia yake ya kutaka kumsajili beki wa Sevilla Jules Kounde wakati wa dirisha hili la majira ya kiangazi lakini sasa beki huyo wa kimataifa wa Ufaransa alipata jeraha alipokuwa kwenye majukumu na timu ya taifa ambapo itamlazimu kufanyiwa upasuaji.
Chelsea hawakufanikiwa kumsajili Kounde mwaka jana lakini safari hii ni kama wanaitaka saini ya Mlinzi huyo baada ya kuondoka Antonio Rudiger na Christensen ambao walikuwa wachezaji muhimu katika mafanikio ya The Blues msimu uliyopita. Lakini jeraha alilopata Kounde huenda likatibua mipango ya Chelsea ya kutaka kumsajili.
Ufaransa wameshindwa kuondoka na ushindi dhidi ya Croatia kwa kukubali kipigo cha 1-0 na sasa wamefikisha idaidi ya mechi nne bila ushindi wakiwa mkiani kwenye jedwali la League A: Group 1 kwenyue michuano ya UEFA Nations League.
Kounde ambaye ana umri wa miaka 23 amjejitambulisha kama moja ya mabeki bora kwa sasa ulimwenguni akiwa sehemu nya mafanikio ya ubingwa wa Europa League msimu wa 2019-20 na Sevilla.
Je, dili itafanikiwa au ndiyo kitumbua kimeingia mchanga baki hapa hapa kuendelea kupata habari motomoto za usajili wakati nwa dirisha hili la Usajili.
ALIYA’S WISHES
Bila shaka unatamani ushindi mkubwa, vipi kuhusu kujaribu Sloti hii ya Aliya’s Wishes? jaribu ushinde sasa.