Kiungo wa Paris Saint-Germain Pablo Sarabia amewahamasisha wachezaji wenzake kutengeneza historia ya timu hiyo kwa kushinda Champions League.
Wababe hao wa Ufaransa hawajawahi kufika hatua ya nusu fainali kwenye michuano hiyo mikubwa ya ulaya ya UEFA.
Tayari wamemalizana na mashindano ya ndani nchini Ufaransa msimu huu sasa wanayageukia mashindano ya Mabingwa Ulaya siku ya Jumatano ikiwa ni hatua ya robo fainali dhidi ya Atalanta jijini Lisbon.
Lakini wakati Sarabia akiwa anahamsisha wenzake, anajua kwamba kukabiliana na Atalanta waliomaliza msimu wakiwa nafasi ya tatu katika ligi ya Serie A, sio shughuli ndogo.
“Ni fursa kubwa, tutajitahidi kufanya iwe kweli na kuweka historia ya Paris Saint-Germain,” alisema kupitia tovuti rasmi ya klabu.
“Nadhani sasa ni muda sahihi wa kutimiza hili, tumekuwa tukilenga hili kimya kimya sasa tuna utayari huo.
“Tutawasoma wapinzani na kuchez kwa hali na mali kuweka historia, nadhani tupo tayari kwa mchezo huu ambao ni muhimu sana tume hamasika kweli.
Kutokana na kuwepo kwa virusi hatari vya Corona msimu huu hatua ya mtoano itakuwa ni ya kipekee kwani michezo yote iliyo salia itapigwa nchini Ureno na kutakua na mzunguko mmoja pekee kuanzia robo fainali na kuendelea.

Kama PSG itafanikiwa kusonga hatua inayofuata basi itakabiliana na RB leipzig au Atletico Madrid kwenye hatua ya nusu fainali, na Sarabia amesema mfumo mpya wa mashindano utakuwa mzuri kwao.
“Tumeshapata kuelewa hali inavyo kwenda, ni mfumo wa kipekee kwa sababu tunaenda kucheza michezo yote sehemu moja, mchezo mmoja, ni kitu ambacho hakijawahi kutokea kabla,” alisema Sarabia.
PSG ambao wapo chini ya kocha Tuchel wanaweza kumkosa mshambuliaji wao Klyan Mbappe kufuatia kupata jeraha kwenye fainali Coupe de la Ligue dhidi ya Lyon.
Umekuwa mteja muaminifu wa meridianbet? Kuna zawadi kibao hadi 5% ya pesa yako inarejeshwa kwako. Kila wiki unaweza kurudishiwa mpaka Tsh 250,000.


Latifa juma mohamed
Safi Sana kujiamini.
David Pere
Ni vigumu sanaa PSG kuchukua UEFA kweli Wana ndoto ya kombe Hilo lakini wafanye kazi kubwa sanaa
Ester jackson
Kwa wakati huu PSG siyo ile ambayo mashabiki tumezoea hii iko tifauti na kuoata kombe wakati huu in kiu yao Mimi nafikiri wanaweza kupata kikubwa ni juhudi.na atletico Madrid mpaka hasaivi hatujui kama itachezwa siku ya ijumaa ya trhe 14 kwa sababu ya wachezaji wake wawili kukutwa na ugonjwa wa corona.
Dorophina
PSG kwa sasa hawana jipya wanajitahidi lkn wameshafeli
Sauda
PSG wafanye kazi kubwa sana ili wapate Kombe
Rose kapinga
Hongera kwanza kwa kujiamini,ila Kaz unayoo!!!!
warda
Nawaombea sana PSG#Meridianbet
Shan
Nice
Mwajumah
PSG kwa sasa hawana jipya#Meridianbettz
rama
Maoni:vizur wachezaj wajitume wote ili waweze kutwaa uefa psg wana muda mrefu hawajachukua kombe hili
Zeiyana
Kwa mwenendo walio kua nao PSG wakiendelea nao asilimia mia wataingia fainali ligi ya mabingwa
Tumaini kasalile
Nice
Sadick
Madhumuni makubwa ya PSG kumununua Neymar na Mbappe ilikuwa kutaka kuwa wafalme wa Ligi hii maarufu barani Ulaya#meridianbettz
magdalena
psg kwa sasa wapambane sana maana hawana jipya tena
Caroline
Mkiamua mnaweza
aisha
Wakaze sana ili wapate hilo kombe
Lydia Emmanuel Magoti
Vizuri sana mkipambana mnaweza PSG
Tatu
Kila kitu kinawezeka mkijiekea malengo sarabia ni MTU wa kujituma ashindwi kitu
Angelina
Goodnews
felister
mkithubutu mnaweza
Leonard
Psg wanaweza kufika hata fainali
Salma ngende
Kujituma zaid kunahitajika
Zuhura omary kindamba
Mkijitahidi mtaweza
Omary lukumbi
Msimu huu unaweza kua bomba kwa psg
Ernest
Psg wanatakiwa wawe makini sana na tatizo lao lingine wanapenda sana kurelax ikumbukwe sasa hakuna home and away wanawaichukulia Atalanta kama timu nyepesi sana
Shafii
Maneno hayajengi Kama fikra za PSG kuchukua club bingwa cha msingi ni kuweka juhudi kubwa Sana hili linaweza likawezekana.
farida ahmadi
Ni vizuri Sana mchezaji kama mchezaji kujiamini hongera Sana Pablo sarabia kwa kujipa imani
Gabriel
Wakiamua kufanya juhud wataweka historia
Flomena
Tumeshapata kuelewa hali inavyo kwenda, ni mfumo wa kipekee kwa sababu tunaenda kucheza michezo yote sehemu moja, mchezo mmoja, ni kitu ambacho hakijawahi kutokea kabla,” alisema Sarabia.
Povel
For me PSG wawape kombe lao
Sabrina
Wapambane tu watapata
Furahav
Ngoja tuone km itakuwa kweli?
Fatuma kasomo
Psg wapambane sana
Hope mwaikuka
Inapendeza sana kujiamin hvyo
Rehema
Good
Adelta
Wanatakiwa wafanye juhudi ili waweze kupata kombe@meridianbettz
Saupha mohamed
PSG wajitume sanaa
Fatina mfingi
Nice
Njiku
PSG ni timu nzuri sana ila wanakuwa na makosa madogo madogo hasa kwa wachezaji kuwa na dharau na timu
Nasra
Ni Jambo zuri Sana Cha msingi waongeze juhudi Kila kitu kitakaa sawa.
Devotha
Good
Samiah
Gud
Mwanahamisi
Wapambane tuu