ALIYEKUWA straika wa Polisi Tanzania, Gerald Mdamu amesema kuwa madaktari wamemsogezea mbele siku za kurejea uwanjani mpaka katikati ya msimu ujao.
Mdamu alivunjika miguu kwenye ajali ya timu hiyo ambayo ilitokea wakati kikosi hicho kikitoka mazoezini kurejea kambini.

Mdamu amesema kuwa “Namshukuru Mungu naendelea vizuri kwa sasa naweza kutembea umbali mrefu.
“Madaktari wameniambia kwa msimu huu naweza kuanza kucheza mpira kuanzia katikati ya msimu. Kwa upande wa viongozi wa Polisi bado nawasikilizia kwani hawajanitafuta kwa ajili ya kuongeza mkataba.”

