Kiingilio cha TZS 3000 katika mchezo wa Simba SC vs Biashara United ni sehemu ya mikakati mipya ya CEO wa klabu hiyo katika kujenga tabia ya wanachama kuingia kila mechi, kukuza mapato kutoka na wengi wataweza kuingia pia ni mkakati wa kuwasoma mashabiki wao au watazamaji kujua kujua shida ipo wapi kutoingia viwanjani katika zile mechi ambazo si za pressure sana ya matokeo.
CEO ni kama anaanza mikakati ya kuibrand klabu kwa pricing strategy. Akifanikiwa hili au kushindwa atakuja na mkakati mwingine ili kuendelea kutoa uzani sawa kwa mshabiki kwa kila mechi ya Ligi au kirafiki. Hapo atakuwa amefanikiwa katika ule mkakati alioutaja wa kukuza mapato (Revenue) kupitia rasilimali watu na vyanzo vingine.
Tuponde kwa dhana ya utani wa jadi na majigambo mengine lakini technically kuna somo kubwa linafanyika.
Soka letu sasa tunalitanua kutoa kwenye ‘pitch’ kuja nje kimkakati. Dakika 90 za uwanjani zinafanikiwa zaidi kutokana na kazi kubwa nje ambayo hugharimu muda , mali na akili za watu. Muunganiko kiutendaji ndio unaleta ufanisi wa dakika 90 zinazochezwa na timu. Kabla ya wachezaji kuingia uwanjani, CEO na line managers wake wote wanatakiwa kufanya kazi kubwa na yenye tija ili kuwapa ufanisi wachezaji. Malipo mazuri, bonus, kuhakikisha branding ya timu na klabu kwa ujumla ipo sawa, kufungua fursa kimasoko na mikakati kabambe ya kila uchao kuvuna rasilimali watu na kuongeza assets za klabu ili kukuza mtaji wake.
Moja ya mikakati hiyo ni hii ya kushusha kiingilio ili kupata volume kubwa ambayo ina faida nyingi kama lengo litafanikiwa. Kwanza kupanda mbegu ya wapenzi, wadau wa soka na mashabiki kwa ujumla kupenda timu yao au soka kwa ujumla. Lile vibe la uwanjani litamfanya na kesho kurudi na mwisho wa siku anapata ile addiction ya kuipenda Simba na soka kiujumla, hivyo kila mechi ataingia hata kama kiwango kitabadilika.
Hizi mechi zinatazamwa duniani kote . Wingi wa mashabiki viwanjani, unawavutia wawekezaji kuja kuwekeza kwakuwa wana uhakika na wingi wa rasilimali watu.
SHINDA NA MERIDIANBET!
Tengeneza pesa kidijitali kwa kubashiri mbio za farasi hapa Meridianbet! Chagua nani ashinde, unakusanya mkwanja.
Cheza Sasa.
Povel
Noma sana hiiiiiii THIS IS SIMBA next level. Twenden kwa MKAPA wakati wetu WAKUWAKERA
magdalena
ni noma sana apo hakuna kukosa ata kidogo
Adelta
Good news 👍😀 @meridianbettz
Nasra
Safi sana wanasimba
Shani
Great madam CEO this plan of yours will make it!! !
Genia Sikaluzwe
Ahsant sana meridianbet kwa taarifa
Mwanahamisi
Gud news
Sauda
Hii si ya kukosa
Njiku
Ipo poa hii
Dorophina
Habari njema kwa mashabiki wa simba watawavuta mashabiki kwa wingi
Antony Luseno
Wazo nzuri kaanza nalo CEO mpya wa klabu ya simba
Lydia Emmanuel Magoti
Mambo yamekuwa juju akuna Kama Simba tukutane kwamkapa ukaone watoto wanavyo ucheza mpila
Fatina
Mambo mazuri kwa club ya simba!!
Zeiyana
Hii itasaidia kwa ali ya uchumi ilivyo polomoka ila kwa Tanzania bado sana tiketi zitaendelea kuuzwa hivyo ivyo kwa bei ile ile kama hawajaweka uwangalizi kwa wauza tiketi wao
Elika
Bora wameweka kiwango kidogo ili mashabiki tujumuike kwa wingi…simba hawanaga kazi mbovu wenyewe wanaridhika na kidogo wanachopata..sisi hatuna maneno eti kujaza uwanja..sisi tunaenda kuangalia mpira
Caroline
Sawa.hicho kiwango watu wengi watamudu
Tatu
CEO wa simba ni mwanadada mrembo na mwenye akili sana kitendo cha kushusha kiingilio hii itatufanya sisi mashabiki kuingia kwa wingi uwanjani pia umeisadia jamii kutoka hali yetu ya uchumi jinsi ulivyo sasa
Mwajumah
Sio kwa kiingilio hicho hakosi mtu apo#Meridianbettz
Ernest
Hapa nimekubali sana hili swala la kupunguza viingilio hasa katika kipindi hiki ulimwengu upo kwenye mapambano na Corona, Salute kwa CEO Mpya Madame mwenye Cv zake
Samira
Mpira ni burudani simba wamejua kutufurahisha wapenzi wa mpira
Saupha mohamed
Mambo safi simbaa
Khadija
Hii si ya kukosa#meridianbettz
Hopemwaikuka
🙊
Fatuma kasomo
Iko pow
Gabriel
C.E.O wa Simba n mrembo sana ninamatumain kazi yake itakuwa nzur
Issa
Senzo atabak kuwa senzo
Salma ngende
Tunasubiri tuone
Sabrina
3000 itapendeza
Tahiya
Ni mwanzo mzur kwa CEO wetu mpya twende tukachangie klabu na uku tunapata burudani
Angelina
Goodnews
Mariam mtandama
Habari njema
Amiri Kayera
Hili ni Jambo zuri
felister
hii si ya kukosa